Afisa Muuguzi Mwandamizi Mstaafu kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mama  Hadija Mradi (kulia) akikata keki wakati wa hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa  Taasisi hiyo ilizopo jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Prof. Mohamed Janabi na kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Uuguzi  Robert Mallya
 Kaimu Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Uuguzi kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert Mallya akimlisha keki Afisa Muuguzi Mwandamizi Mstaafu Mama  Hadija Mradi wakati wa hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika leo katika  ukumbi wa mikutano wa  Taasisi hiyo uliopo jijini Dar es Salaam . Anayeshuhudia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Prof. Mohamed Janabi.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Prof. Mohamed Janabi (kushoto) akimkabidhi cheti cha kutambua mchango wake katika utumishi wa umma kwa kufanya kazi kwa miaka 41 Afisa Muuguzi Mwandamizi Mstaafu Mama  Hadija Mradi katika  hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Uuguzi Robert Mallya.
 Afisa Muuguzi Mwandamizi Mstaafu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mama  Hadija Mradi (kulia) akifuatilia yaliyokua yakiendelea wakati wa hafla fupi ya kumuaga iliyofanyika leo katika Taasisi hiyo. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo Delila Kimambo.
Baadhi ya wafanyakazi  wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia matukio mbalimbali yaliyokua yakiendelea wakati wa hafla fupi ya kumuaga Afisa Muuguzi Mwandamizi Mstaafu Hadija Mradi (hayupo pichani) iliyofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo uliopo jijini Dar es Salaam. Picha na JKCI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...