Na Veronica Simba – Morogoro
Wananchi wa Kijiji cha Mtego wa Simba, Kata ya Mikese, Wilaya ya Morogoro Vijijini, wameshindwa kuzuia furaha yao baada ya Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu, kuzindua rasmi uwashaji wa umeme katika Kijiji hicho, kupitia Mradi wa Umeme Vijijini, Awamu ya Tatu, Mzunguko wa Kwanza (REA IIIA.)
Tukio hilo la kuwasha umeme, lilifanyika Jumatano, Julai 11, 2018 na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mjini, Regina Chonjo ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa, Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki, Omari Mgumba, Madiwani na Wenyeviti wa Vijiji.
Akizungumza kwa niaba ya wananchi, ambao muda wote walionesha bashasha, Mgumba ambaye pia ni Naibu Waziri wa Kilimo, aliishukuru Serikali kupitia Wizara ya Nishati, kwa kuendelea kutekeleza ahadi ya kuwapelekea wananchi, hususan walioko vijijini nishati ya umeme.
“Serikali iliahidi kwamba itasambaza umeme kwa vijiji vyote vilivyobaki, kwenye Awamu mbili za REA III. Tunatoa shukrani sana kwa kuja hapa leo kutekeleza ahadi hiyo kwa vitendo.”
Akizungumza katika Hafla hiyo, Naibu Waziri aliwaeleza wananchi kuwa baada ya uzinduzi huo, wataanza kuunganishiwa umeme katika nyumba zao kuanzia Ijumaa, Julai 13, mwaka huu.
“Nimeongea na Mkandarasi, kuanzia Ijumaa, zile nyumba za awali 62 zote zitawekewa umeme.”
 Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (katikati) akifurahia baada ya kukata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa uwashaji umeme katika kijiji cha Mtego wa Simba, Kata ya Mikese, Wilaya ya Morogoro Vijijini, Jumatano, Julai 11, 2018. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mjini, Regina Chonjo na wa kwanza kulia ni Naibu Waziri wa Kilimo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki, Omari Mgumba.
 Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akizungumza wakati wa Hafla ya uzinduzi rasmi wa uwashaji umeme katika kijiji cha Mtego wa Simba, Kata ya Mikese, Wilaya ya Morogoro Vijijini, Jumatano, Julai 11, 2018.
 Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (katikati) akiwasha taa ya umeme, katika moja ya vyumba vya Zahanati ya Kijiji cha Towero, Kata ya Mlimani, Wilaya ya Morogoro Mjini, Jumatano, Julai 11, 2018. Naibu Waziri alitembelea Zahanati hiyo kujiridhisha endapo agizo alilotoa kwa TANESCO kuiunganishia umeme limetekelezwa. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mjini, Regina Chonjo na wa kwanza kulia ni Meneja wa TANESCO wa Kanda ya Kati, Mhandisi Athanas Nangali.
 Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu, akiwaonesha wananchi wa Kijiji cha Mtego wa Simba, Kata ya Mikese, Wilaya ya Morogoro Vijijini, kifaa kitumikacho kuwasha umeme pasipo kutandaza nyaya katika nyumba, kijulikanacho kama Umeme Tayari (UMETA). Alikuwa katika ziara ya kazi kijijini hapo ambapo alizindua rasmi uwashaji wa huduma ya umeme, Jumatano, Julai 11, 2018.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...