Wananchi wa eneo la Buza katika Manispaa ya Temeke Jijini Dar es salaam wameishukuru serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais John Magufuli kwa ujenzi wa kituo cha afya Buza. 

Shukrani hizo wamezitoa leo wakati Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo alipofanya ziara ya kushtukiza kituoni akiwa safarini kuelekea wilayani Kibaha kukagua miradi ya maendeleo. 

Alipofika kituoni hapo, Waziri huyo alikutana na umati wa kinamama na watoto wakisubiri kupata huduma katika Majengo yenye changamoto kubwa. Akizungumza na wananchi na wagonjwa waliokuwepo Kituoni hapo, Waziri Jafo amesema ameamua kufanya ziara hiyo ili kujionea hali halisi ya wananchi hao wanavyopata huduma ya afya. 

“Serikali inatambua changamoto zinazowakabili lakini nimeleta habari njema kwenu kuwa serikali itakiboresha kituo hicho ili kuondoa kero zinazowakabili,”amesema.Ameeleza kuwa kituo hicho kitajengewa jengo la upasuaji, wodi, maabara, jengo la wagonjwa wa nje ikijumuisha vyumba vya madaktari pamoja na jengo la X-Ray na mradi unaotarajiwa kugharimu zaidi ya sh.Bilioni moja.

Kufuatia hali hiyo, Wananchi hao wameishukuru serikali kwa kuendelea kutatua changamoto zinazowakabili na kwamba uboreshaji huo utawawezesha waweze kupata huduma bora za afya.
Wananchi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo(hayupo pichani) alipofanya ziara ya kukagua utoaji wa huduma katika zahanati ya Buza.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo akizungumza na wananchi alipokuwa akikagua utoaji wa huduma katika zahanati ya Buza.
Wananchi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo(hayupo pichani).
Wananchi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo(hayupo pichani) alipofanya ziara ya kukagua utoaji wa huduma katika zahanati ya Buza.
Wananchi wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Selemani Jafo(hayupo pichani) alipofanya ziara ya kukagua utoaji wa huduma katika zahanati ya Buza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...