Mkazi wa Morogoro, Frank Kisayo ameshinda zawadi ya televisheni ya kisasa aina ya Samsung yenye ukubwa wa inchi 32 kupitia promosheni ya Amsha Amsha Ushinde na Airtel Money ambayo inaendeshwa kampuni ya simu ya Airtel Tanzania na kampuni ya michezo ya kubashiri ya SportPesa.

Kisayo ambaye ni mkulima, alishinda televisheni hiyo kwenye droo ya tatu iliyofanyika kwenye Ofisi Makao Makuu ya Ofisi za kampuni ya simu ya Airtel jijini.

Akizungumza kwa njia ya simu mara baada kushinda droo hiyo, Kisayo alisema kuwa amefurahi sana kushinda zawadi hiyo yenye thamani si chini ya Sh750,000.

“Siamini kama nimeshinda, nasubiri kwa hamu zawadi yangu, naamini sasa suala la kununua televisheni kwangu limeisha baada ya kushinda zawadi hii nono ya droo ya Amsha Amsha,” alisema Kisayo.

Mbali ya Kisayo, pia Masoud Saleh wa Kisarawe  na Shadrack Sanga wa Manyara kila mmoja alishinda simu ya mkononi aina ya Samsung Galaxy yenye thamani Sh500,000.

Pia Eric  Samwel ambaye ni mkazi wa Tanga alijishindia jezi na tiketi ya msimu ya kuona mechi ya Yanga na Simba za msimu ujao.

Maneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando alisema kuwa mpaka sasa washindi watatu wa televisheni, simu 25 na jezi 25 wamepatikana katika droo hiyo.
Meneja Matukio wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Dangio Kaniki, akiongea na moja ya washindi wa AMSHA AMSHA USHINDE NA AIRTEL MONEY kwa kushirikiana na Sportpesa, Dar es Salaam jana. Kulia ni Meneja Uhusiano Sabrina Msuya Kushiriki, mteja atatakiwa kupiga *150*60# kisha kutuma pesa kwenye akaunti ya SportPesa namba 150888 kisha kuweka kubashiri.
Meneja Uhusiano SportPesa Sabrina Msuya, akiongea na moja ya washindi wa AMSHA AMSHA USHINDE NA AIRTEL MONEY kwa kushirikiana na Sportpesa, Dar es Salaam jana. Kulia ni Meneja Matukio Airtel Tanzania. Mteja atatakiwa kupiga *150*60# kisha kutuma pesa kwenye akaunti ya SportPesa namba 150888 kisha kuweka kubashiri.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...