Na .WAMJW-Tabora
Serikali
kupitia Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto
inatarajia kupeleka shilingi milioni 300 kwenye hospitali ya rufaa ya
Mkoa ya Kitete kwa ajili ya kupanua wodi ya wazazi pamoja na ununuzi wa
vifaa vya upasuaji kwa kumtoa mtoto tumboni Mkoani humo
Hayo
yamesemwa na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto
Ummy Mwalimu wakati alipotembelea hospitali hiyo ziara ya kikazi mkoani
hapa.
"tutaleta
fedha hizi kabla ya desemba mwaka huu ili kuhakikisha kila mwanamke
mjamzito anajifungua salama na mtoto wake anakua salama pia"alisema
Waziri Ummy.Aidha,aliwaagiza
hospitali hiyo kununua vifaa vyote muhimu vinavyowezekana kuliko
kusubiri wizara iwaletee'lazima mjiongeze na kuwa wabunifu muwe na vitu
muhimu ili msonge mbele'alisisitiza
Hata
hivyo aliwataka watumishi hao kufanya kazi kwa kuzingatia maadili na
miiko ya utumishi wa umma ili kuondoka malalamiko kwa wananchi wanaofika
kupata huduma katika hospitali hiyo.
Picha jengo la upasuaji lililopo katika hospitali hiyo
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt.Gunini Kamba akimueleza Waziri wa Afya vifaa vilivyofungwa kwenye chumba cha upasuaji vilivyofungwa kwenye jengo la Upasuaji lililojengwa hospitalini hapo
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akimbeba mtoto mchanga aliyezaliwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Kitete Mkoani Tabora
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt.Gunini Kamba akimueleza Waziri wa Afya vifaa vilivyofungwa kwenye chumba cha upasuaji vilivyofungwa kwenye jengo la Upasuaji lililojengwa hospitalini hapo
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akimbeba mtoto mchanga aliyezaliwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Kitete Mkoani Tabora
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...