Na .WAMJW-Tabora

Serikali kupitia Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto inatarajia kupeleka shilingi milioni 300 kwenye hospitali ya rufaa ya Mkoa ya Kitete kwa ajili ya kupanua wodi ya wazazi pamoja na ununuzi wa vifaa vya upasuaji kwa kumtoa mtoto tumboni Mkoani humo

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati alipotembelea hospitali hiyo ziara ya kikazi mkoani hapa.

"tutaleta fedha hizi kabla ya desemba mwaka huu ili kuhakikisha kila mwanamke mjamzito anajifungua salama na mtoto wake anakua salama pia"alisema Waziri Ummy.Aidha,aliwaagiza hospitali hiyo kununua vifaa vyote muhimu vinavyowezekana kuliko kusubiri wizara iwaletee'lazima mjiongeze na kuwa wabunifu muwe na vitu muhimu ili msonge mbele'alisisitiza

Hata hivyo aliwataka watumishi hao kufanya kazi kwa kuzingatia maadili na miiko ya utumishi wa umma ili kuondoka malalamiko kwa wananchi wanaofika kupata huduma katika hospitali hiyo.
 Picha jengo la upasuaji lililopo katika hospitali hiyo
 Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt.Gunini Kamba akimueleza Waziri wa Afya vifaa vilivyofungwa kwenye chumba cha upasuaji vilivyofungwa kwenye jengo la Upasuaji lililojengwa hospitalini hapo
 Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akimbeba mtoto mchanga aliyezaliwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Kitete Mkoani Tabora

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...