Jumla ya walengwa 3,955 wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini unaotekelezwa na Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii –TASAF wanaendelea kunufaika na mpango huo katika Manispaa ya Shinyanga.

Hayo yamebainishwa jana Agosti 9,2018 na Mratibu wa Kunusuru Kaya Maskini - TASAF Manispaa ya Shinyanga Octavina Kiwone akizungumza na waandishi wa habari.

Kiwone alisema Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika manispaa ya Shinyanga ulianza kutekelezwa mwaka 2015 ukiwa na walengwa 4,244 ambao hata hivyo walipungua kutokana na wengine kufariki na wengine tuliwaondoa kwa kukosa sifa za kuwa kwenye mpango lakini mpaka sasa tuna walengwa 3,955,

"Tangu mwaka 2015 mpaka sasa tumepokea fedha za serikali jumla ya shilingi bilioni 3,fedha ambazo tumewapa walengwa ni shilingi bilioni 2.7 na tayari zimewafikia walengwa ambapo fedha hizi zinawasaidia kwa sababu wanapewa fedha kisha kufundishwa namna ya kutumia fedha hizo",alifafanua.
Mratibu wa Kunusuru Kaya Maskini - TASAF Manispaa ya Shinyanga Octavina Kiwone akizungumza na waandishi wa habari.- Picha na Kadama Malunde - Malunde1 blog.KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...