Ilikuwa katika viwanja vya maonyesho ya International Afrika Festival Tübingen nchini ujerumani ambapo katika maonyesho hayo mwaka huu 2018 nchi lengwa ilikuwa ni Tanzania na mgeni wa heshima rasmi alikuwa balozi wa Tanzania nchini ujerumani mheshimiwa dkt. Abdallah Possi ambaye alihutubia ummati wa kadamnasi ya waudhuriaji wakiwemo wawekezaji kuwa Tanzania kuna fursa kubwa za uwekezaji na pia nchi salama.

onyesho hilo kubwa lilinogeshwa na bendi za muziki kama Ngoma Africa band maarufu FFU-Ughaibuni inayoongozwa na kamanda Ras Makunja,bendi ya Mvula-Mandondo Band inayoongozwa na msanii Saidi Kanda yenye maskani kule Uingereza nayo ilifanya vizuri,wasanii wa kizazi kipya kama Nashi MC kutoka Tanzania naye alitingisha jukwaa msanii wa picha za kuchora Chilonga Haji naye alikuwa moja ya waonyeshaji wa bidhaa toka Tanzania.onyesho lilifana sana sana na kuitanga za Tanzania kimataifa.
Balozi wa Tanzania nchini Ujermani Mhe. Dk. Abdallah Possi akiwa na wawekezaji wakiangalia naadhi ya bidhaa katika maonyesho mjini Tubingen,Ujerumani.
Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Dk. Abbdalaah Possi akiwa katika maonyesho ya Gaiexpo mjini Tubingen,mwaka huu nchi lengwa ilikuwa Tanzania.
Ngoma Africa Band wakiwa jukwaani katika onyesho la Tubingen.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...