Na Dixon Busagaga ,Moshi.
MGOMBEA udiwani katika kata ya Mawenzi ,manispaa ya Moshi ,Apaikunda Naburi (CCM) amefanikiwa kushinda nafasi hiyo akiwashinda wagombea wengine baada ya kupata kura 400 sawa na asilimia 70.3 kati ya kura 569 zilizopigwa.
MGOMBEA udiwani katika kata ya Mawenzi ,manispaa ya Moshi ,Apaikunda Naburi (CCM) amefanikiwa kushinda nafasi hiyo akiwashinda wagombea wengine baada ya kupata kura 400 sawa na asilimia 70.3 kati ya kura 569 zilizopigwa.
Naburi aliyekuwa diwani wa kata ya Mawenzi katika kipindi cha mwaka 2010-2015 kabla ya kushindwa na aliyekuwa Diwani wa kata hiyo ,Hawa Mushi aliyefariki dunia hivi karibuni baada ya kuugua ghafla.Mgombea huyo amefanikiwa kurejea kwenye nafasi hiyo kwa kuwashinda Afrikana Mlay wa Chadema na na Isaac Kereti wa SAU waliokuwa wakiwania kiti hicho.
Akitangaza matokeo ya uchaguzi msimamizi wa uchaguzi , Erasmo Silayo alimtangaza Naburi kuwa mshindi halali wa kiti hicho huku akitaja kura za mgombea aliyefuatia kuwa ni Afrikana Mlay (Chadema) aliyepata kura 163 huku mgombea Isack Kireti (SAU) akiambulia kura 2.
.Akizungumza mara baada ya kutangazwa mshindi,Naburi amewashukuru wapiga kura katika kata hio huku akiwaahidi ushirikiano katika kuwatumikia.
"Idadi ya wapiga kura waliojiandikisha ni 1821, kati yao idadi halisi ya wapiga kura ni 569 ambapo kura 4 ziliharibika"alisema Silayo.
Msimamizi
wa uchaguzi , Erasmo Silayo akimtangaza Naburi kuwa mshindi halali wa
kiti hicho huku akitaja kura za mgombea aliyefuatia kuwa ni Afrikana
Mlay (Chadema) aliyepata kura 163 huku mgombea Isack Kireti (SAU)
akiambulia kura 2.
Msimamizi
wa uchaguzi , Erasmo Silayo akimkabidhi cheti cha ushindi kwa Naburi mara baada ya kutangazwa mshindi halali wa
kiti hicho huku akitaja kura za mgombea aliyefuatia kuwa ni Afrikana
Mlay (Chadema) aliyepata kura 163 huku mgombea Isack Kireti (SAU)
akiambulia kura 2.
MGOMBEA
udiwani katika kata ya Mawenzi ,manispaa ya Moshi ,Apaikunda Naburi
(CCM) akionesha cheti chake mara baada ya kushinda nafasi hiyo akiwashinda wagombea wengine
baada ya kupata kura 400 sawa na asilimia 70.3 kati ya kura 569
zilizopigwa.
Wakisherehekea ushindi wao mara baada ya kutangazwa mshindi
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...