Na Mwamvua Mwinyi ,Kibaha Vijijini

MBUNGE wa jimbo la Kibaha Vijijini ,Hamoud Jumaa amekabidhi gari la wagonjwa (ambulance ),iliyogharimu mil.75 ,katika kituo cha afya cha Kwala .

Gari hiyo itaendelea kusaidia kupunguza adha ya usafiri kwa wagonjwa hasa mahututi na warufaa.Akikabidhi gari hilo ,kwa mganga mfawidhi wa kituo hicho ,diwani wa kata ya Kwala, mbele ya wananchi ,Jumaa alisema ataendelea kuwatumikia wananchi na kutatua kero zao .

"Serikali yetu inafanya makubwa katika kupunguza changamoto mbalimbali kwenye sekta ya afya na nyingine kama elimu ,miundombinu na nishati ya umeme""Kwa kutambua hayo ,July 2017 nilikabidhi magari mawili ya wagonjwa yaliyotokana na mfuko wangu na jingine moja ni msaada kutoka kwa Rais John Magufuli ikiwa ni kati ya magari ya wagonjwa 67 yaliyogawanywa katika maeneo mbalimbali nchini" alisema Jumaa.

Hata hivyo Jumaa ,alisema ameamua kujikita kutatua kero mbalimbali ili kwenda pamoja na kauli mbiu yake ya SISI KWANZA SERIKALI BAADAE .Mbunge huyo ,aliomba magari hayo yatunzwe na kutumike kwa matumizi lengwa.Nae mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kibaha,ambae pia ni diwani wa Kwala , Mansoor Kisebengo ,alisema hairuhusiwi wananchi kugharamia mafuta kwenye magari hayo .

Alielezea, halmashauri hiyo imekuwa inachangia gharama za mahitaji ya mafuta ili kuondoa bugudha kwa wananchi .Kwa upande wake mganga mfawidhi kituo cha afya Kwala ,dk.Mustapha Jaffar alimshukuru mbunge huyo kwa msaada alioutoa .Alisema hajafanya makosa kupeleka gari eneo la Kwala ,kwani litakuwa msaada mkubwa kwa wajawazito na wagonjwa wa rufaa.
Mbunge wa jimbo la Kibaha Vijijini ,Hamoud Jumaa akikabidhi funguo ya gari la wagonjwa ambalo limegharimu mil.75 ,kwa mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kibaha ,Mansoor Kisebengo ambae pia ni diwani wa kata ya Kwala.(picha na Mwamvua Mwinyi)
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kibaha ,Mansoor Kisebengo ambae pia ni diwani wa kata ya Kwala, akizungumza na wananchi wa Kwala ,kabla ya mbunge wa jimbo la Kibaha Vijijini ,Hamoud Jumaa kukabidhi gari la wagonjwa ambalo limegharimu mil.75 ,kwenye Kituo cha afya cha Kwala.(picha na Mwamvua Mwinyi)
Mbunge wa jimbo la Kibaha Vijijini ,Hamoud Jumaa akizungumza na wananchi wa Kwala kabla ya kukabidhi gari la wagonjwa ambalo limegharimu mil.75 ,katika kituo cha afya cha Kwala.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...