Dar es Salaam - Agosti 10, 2018. Waumini wa dini ya Kiislamu nchini na duniani kote wanatarajia kusherehekea sikukuu ya Eid Al Adha siku ya Jumanne ya tarehe 21 mwezi wa Agosti. Hata hivyo, hii ni tarehe inayokadiriwa kwa sababu siku rasmi inaweza kubadilika kutegemeana na kuonekana kwa mwezi wa Dhul Hijjah.

Eid Al Adha ni sikukuu ambayo husherehekewa na miongoni mwa Waislamu duniani kote katika kukumbuka sadaka aliyoitoa Nabii Ibrahim (AS) kutokana na imani aliyokuwa nayo kwa mwenyezi Mungu (SWT). Nabii Ibrahim alionyesha utayari wake wa kumtoa sadaka mwanaye wa pekee, Ismail, lakini baadaye Mungu alimtoa mwanakondoo ili awe mbadala wa sadaka. Mwenyezi Mungu alipendezwa sana na usikivu wa Ibrahim kwake na kuwataka Waislamu kukifanya kitendo hiki na imani iliyoonyeshwa kuwa sehemu ya maisha yao.

Hivyo basi, kila mwaka ifikapo siku ya 10 ya mwezi wa Dhul Hijjah, Waislamu wote duniani husherehekea sikukuu ya Eid Al Adha. Katika siku hii, Waislamu huchinja mwanakondoo, mbuzi, kondoo, ng’ombe au ngamia kuheshimu kitendo kilichofanywa na Ibrahim. Sherehe hii hutawaliwa na matendo ya ukarimu na shukrani.
Katika kunogesha shamrashamra za sikukuu hii ya Eid, Jumia Tanzania, kampuni inayojishughulisha na utoaji wa huduma za manunuzi ya bidhaa kwa njia ya mtandaoni, imeamua kujumuika na wateja wake kwa kutoa mbuzi bure ili kufanikisha azma zao.

Mbuzi hao watatolewa kwa namna ya kipekee kabisa ambapo wateja watahitajika kutembelea tovuti ya Jumia ili kujishindia. Mbuzi watafichwa kwenye bidhaa tofauti zinazopatikana mtandaoni na mteja atakayefanikiwa kumtafuta mpaka akampata atakuwa ndiye mshindi halali. Washindi wote watapigiwa simu mara baada ya kushinda na kukabidhiwa hadharani.

Zoezi hilo litafanyika kwa kipindi cha wiki yote ijayo kuanzia Agosti 16 mpaka 20 ili kutoa fursa ya kuwakabidhi mbuzi wao na kuendelea na maandalizi ya sherehe za sikukuu ya Eid. Kwa kila siku ya shindano mteja mmoja ataweza kujishindia mbuzi mmoja aliyefichwa kwenye miongoni mwa bidhaa zilizomo kwenye mtandao wa Jumia. Vivyo hivyo kwa siku zitakazofuatia mpaka mwisho wa kampeni.
“Eid Al Adha au Eid ya kuchinja kama inavyofahamika na wengi pia ni sikukuu muhimu kwa ndugu zetu Waislamu. Tunafahamu kuwa sio watu wote wanao uwezo wa kununua mnyama wa kuchinja siku hiyo hivyo tumeona ni vema kutoa fursa kulifanikisha hilo,” alisema na kuhitimisha Afisa Uhusiano wa Umma wa kampuni hiyo, Hadijah Natalia Tuwano, “nawasihi wateja wetu kujaribu bahati yao kwa kucheza ili kushinda mbuzi kwa ajili ya sikukuu ya Eid. Fursa hii ni kwa wateja wote bila ya upendeleo wowote. Tunawatakia kila la kheri wote watakaoshiriki katika zoezi hili na ikiwezekana kuwaalika na wenzao, tunaamini litakuwa na manufaa kwao, familia, ndugu na jamaa zao.”

Sikukuu ya Eid Al Adha inalenga kumfanya Muislamu kutenda mema zaidi na kujipima na matendo yake. Haitakiwi kutoa sadaka pekee; bali inamaanisha kujifunza masomo yaliyojificha ndani yake ambayo ni kuwa huru dhidi ya matamanio ya kwa mbinafsi, na kumuinua Muislamu dhidi ya chochote kinachokwamisha uwezo wake wa kutekeleza majukumu yake kama Muislamu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...