Mkuu wa wilaya Uvinza Mwanamvua Mrindoko (wa nane kushoto) kwa niaba ya Mkuu wa mkoa Kigoma Emanuel Maganga (hayupo pichani) akipokea kwa pamoja na wadau na watumishi mbalimbali msaada kutoka kwa Mkuu wa masoko na mawasiliano wa Benki ya Exim Stanley Kafu (wa nne kulia) wa vitanda na magodogoro 50 yaliyotolewa na Benki ya Exim kusaidia upungufu wa vitanda kwenye hospitali ya rufaa ya mkoa Kigoma Maweni. Hospitali ya Maweni mkoani Kigoma ni hospitali ya kumi na mbili kupata msaada wa vitanda na magodoro kutoka Benki ya Exim Tanzania.
Baadhi ya watumishi na wadau mbalimbali waliohudhuria tukio la Benk ya Exim kukabidhi vitanda na magodoro kwa hospitali ya mkoa Kigoma Maweni.
Mkuu
wa wilaya Uvinza, Mwanamvua Mrindoko (aliyesimama katikati)
akizungumza muda mfupi kabla hajapokea kwa niaba ya Mkuu wa mkoa Kigoma,
Emanuel Maganga (hayupo pichani) msaada wa vitanda na magodogoro 50
yaliyotolewa na Benki ya Exim kusaidia upungufu wa vitanda kwenye
hospitali ya rufaa ya mkoa Kigoma Maweni. Wa pili kulia ni Mkuu wa
masoko na mawasiliano wa Benki ya Exim Stanley Kafu (na kushoto) ni
Katibu Tawala wa mkoa Kigoma Shaban Mchata.
BENKI ya Exim Tanzania leo katika kukamilisha kampeni yake
ya miaka 20 ya kujali jamii imekabidhi vitanda na magodoro 50 kwa Hospitali ya
Maweni mkoani Kigoma. Benki ya Exim Tanzania iliadhimisha miaka 20 ya huduma,
mwezi wa Agosti mwaka jana, kwa kuzindua mradi wa mwaka mzima unaoitwa “miaka 20 ya kujali jamii” ambao Benki
hiyo imewekeza shilling milioni 200 katika sekta ya afya Tanzania hasa kwenye kuboresha
huduma za afya zinazotolewa kwa wakina mama na wanawake.
Hospitali na kliniki nyingi nchini zina
tatizo la ukosefu wa dawa, vifaa na vitanda hasa katika hospitali za rufaa. Katika
kukabiliana na uhaba huu unaosumbua taifa, benki ya Exim Tanzania, yenye uwepo
wa kimataifa imeanzisha mradi unaolenga kusaidia upungufu wa vitanda katika
wodi za wazazi kwenye hospitali nchini - hivyo benki ya Exim itatoa magodoro
and vitanda 500 katika hospitali za serikali k
atika mikoa mbali mbali nchini
kama sehemu ya kampeni yake ya mwaka yenye lengo la kusherehekea miaka 20 ya
kutumikia jamii.
Hospitali ya Mkoa wa Kigoma ya Maweni
ni hospital ya kumi na mbili kupokea mchango huu, baada ya hospital ya Mawenzi
mkoani Kilimanjaro mwezi Juni, hospitali ya serikali ya Sekou Toure ya mkoani Mwanza
mwezi Mai, hospitali ya rufaa ya Morogoro mwezi Aprili, hospitali ya rufaa ya
Mwananyamala mkoani Dar es Salaam mwezi Machi, hospitali ya rufaa ya Bombo, mkoani Tanga mwezi Febuari,
hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Mbeya mwezi Januari, hospitali ya Mount Meru,
Arusha mwezi Desemba, Hospital ya rufaa Dodoma mwezi Novemba, hospitali ya
rufaa Ligula, Mtwara mwezi Oktoba, Hospitali ya Mnazi Mmoja, Unguja, Zanzibar
mwezi Septemba na Hospitali ya rufaa Temeke, Dar es Salaam mwezi wa nane mwaka
jana.
Tukio lilifanyika kwenye hospitali hiyo katika wodi ya wazazi na mgeni
rasmi alikuwa Mkuu wa wilaya ya Uvinza, Kigoma Mwanamvua Mrindoko, Mkuu wa
idara ya masoko na mawasiliano wa benki ya Exim Tanzania, Stanley Kafu na
Mkurugenzi wa hospital ya Maweni mkoani Kigoma Dk. Osimund
Dyegura.
Mkurugenzi wa hospital ya Maweni mkoani
Kigoma, Dk. Osimund Dyegura alipongeza Exim Bank Tanzania kwa msaada wake na
kuhimiza taasisi mbalimbali kutekeleza ishara ya Benki ya Exim Tanzania katika
kusaidia kuboresha huduma ya afya kwa nchini. Aliongezea kwa kusema “Upungufu
wa vitanda katika mahospitali ni changamoto kubwa. Msaada huu kutoka benki ya
Exim wa hivi vitanda 50 na magodoro utasaidia sana katika kupunguza changamoto
hii.”
Akizungumza katika hafla hiyo ya
makabidhiano, Mkuu wa idara ya masoko na mawasiliano wa benki ya Exim Tanzania,
Stanley Kafu alisema, “Benki imetambua umuhimu wa jumuiya zinazozunguka eneo la
biashara yetu na ndio maana shughuli za kijamii ni muhimu sana kwa Benki ya
Exim. Tunaamini kwamba tuna sehemu kubwa katika kufanya mabadiliko mazuri
katika sekta mbalimbali katika jamii zetu.
Ni kwa hili Benki iliamua
kusherehekea miaka 20 kwa kusaidia jamii kwa njia ya kampeni inayoitwa, “miaka 20 ya kujali jamii” kuonyesha jinsi
tunavyowashukuru. Japokuwa mradi huu umefikiwa ukingoni Benki ya Exim itaendelea
kutoa misaada katika sekta ya afya kwenye hospital mbali mbali nchini.”
Benki ya Exim ilitambuliwa kama benki
bora kwa huduma ya wateja binafsi mwaka 2017 inasheherekea miaka 20 ya
mafanikio, ukuaji na kuwa kiongozi katika kuingia katika masoko mapya barani
Afrika. Benki ya Exim ilianzishwa mwaka 1997 na imetanua soko lake kwa kufungua
kampuni tanzu katika nchi za Comorro (2007), Djibouti (2010) na Uganda (2016).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...