Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mh Anthony Peter Mavunde ameahidi kutoa usafiri bure kwa wananchi wa Jimbo la Dodoma Mjini watakaopata misiba kwa kutoa gari ambalo litakaa eneo la kuhifadhia miili ya Marehemu “ MORTUARY” mahsusi kwa ajili ya kusafirisha miili ya marehemu na waombelezaji.

Mavunde ameyasema hayo leo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma alipoongoza maelfu ya wananchi wa Dodoma katika uzoezi la upimaji macho katika kambi maalum iliyoandaliwa kwa ushirikiano wa Ofisi ya Mbunge Dodoma Mjini,Lions Club Mzizima na Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma ambapo wananchi wanapata huduma ya bute ya upimaji macho,kupatiwa miwani na kufanyiwa upasuaji wa jicho.

Aidha,Mh Mavunde amewashukuru sana Lions Club Mzizima kwa kutoa huduma hiyo kwa wananchi wake na kuwaomba wasisite kuendelea kutoa huduma hiyo pindi watakapohitajika wakati mwingine kwa kuwa matatizo ya mtoto wa jicho ni kati ya matatizo makubwa yanayowaathiri wananchi wengi wa mkoa wa Dodoma.
Baadhi ya Wakazi wa Dodoma waliojitokeza kwa wingi leo kwenye hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma wakiongozwa na Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mh Anthony Peter Mavunde katika uzoezi la upimaji macho katika kambi maalum iliyoandaliwa kwa ushirikiano wa Ofisi ya Mbunge Dodoma Mjini,Lions Club Mzizima na Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma
Mbunge wa Dodoma Mjini Mh Anthony Mavunde akipata maelezo kutoka kwa Viongozi wa Mzizima Lions Club
Mbunge wa Dodoma Mjini Mh Anthony Mavunde akisalimiana na baadi ya Viongozi wa Mzizima Lions Club

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...