KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Mhandisi Charles Francis Kabeho amefungua Jengo la Ofisi za Shirika la Umeme nchini (Tanesco) wilayani Bahi mkoani Dodoma ikiwa ni mpango wao wa kusogeza huduma karibu na wananchi waliopo maeneo mbalimbali hapa nchini. 

Akizungumza mara baada ya kufungua Jengo hilo Mhandisi Kabeho amepongeza juhudi zinazofanywa na shirika hilo katika kuhakikisha ofisi zao zipo kwenye mazingira mazuri ya wafanyakazi kuweza kuwahudumia wananchi kwa ufanisi wakati wanapokuwa wakifika kwenye maeneo yao kupata huduma .Alisema hatua ya wao kupanua wigo mpana wa kuwafikia wananchi itawawezesha kuondokana na changamoto mbalimbali ikiwemo kuzifuata kwa umbali mrefu hivyo jambo hilo linahitaji kupongezwa kutokana na kuona umuhimu wa kuwafikia 

“Nimependezwa na jitihada za TANESCO katika kuhakikisha wateja wanafiki wa na huduma za Umeme kwa ukaribu zaidi, nakuhudumiwa katika mazingira mazuri, hivyo niwapongeze TANESCO kwa hili lakini pia nisistize kuwa ofisi hizi ziweze kuhudumia wateja hao kwa weledi”alisemaMhandisi Kabeho .Naye Mkuuwa Wilaya ya Bahi Mwanahamisi Mkunda amemshukuru Mkuuwa Mbioza Mwenge kwa kuweza kufungua jingo hilo na kuwa hakikishia wananchi wa Bahi kuwa Huduma ya umeme sasa ipo karibu na kuwa wilaya ya Bahi sasa inauhakika wakupata hudumaza Umeme masaa 24, 

Kwa upande wake Meneja wa TANESCO wilaya ya Bahi, Mhandisi Bryceson Kitila amesema kuwaUjenzi wa jengo la Ofisi ya Bahi umetekelezwa naShirika la Umeme Tanzania kwa madhumuni ya kuongeza Ufanisi wakazi katika mji wa Bahi na vijiji vya Jirani,pia kuwezesha wananchi wa Bahi kupata Huduma Bora nayaUhakika kwa kuwa na kituo cha huduma kwa wateja(one stop shop center) hivyo mteja anaweza kupata huduma zote katika dawati moja ikiwemo na manunuzi ya umeme (LUKU). 

Mbio hizi za Mwenge wa Uhuru, zimehitimishwa katika mkoawa Dodoma ambapo zimehusishau funguaji wa miradi mbalimbali ya Maendeleo ikiwemo Jengo la TANESCO.
 MKUU wa wilaya ya Bahi Mwanahamisi Mkunda akitoa shukrani kwa KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Mhandisi Charles Francis Kabeho kushoto mara baada ya uzinduzi wa Jengo la Tanesco wilaya ya Bahi 
 MKUU wa wilaya ya Bahi Mwanahamisi Mkunda kulia akiwa na KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Mhandisi Charles Francis Kabeho kushoto mara baada ya uzinduzi wa Jengo la Tanesco wilaya ya Bahi 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...