MSTAHIKI Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita leo amefanya ziara katika hospitali ya Aga Khan ya jijini hapa na kuwaona wagaonjwa sambamba na kupata nafasi ya kuona maendeleo ya mradi wa upanuzi wa hospitali hiyo ulio mbioni kukamilika .

Katika ziara hiyo , Meya Mwita amekutana na uongozi wa juu wa Hospitali hiyo ikiongozwa na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Utoaji Huduma za Afya Aga Khan Kanda ya Afrika Mashariki, Sulaiman Shahabuddin ambapo walipata nafasi ya kuzungzumza mambo mbalimbali.

Meya Mwita ameipongeza Taasisi ya Huduma za Afya Aga Khan Tanzania kwa kuamua kuwekeza katika Mkoa wa Dar es Salaam hususani sekta ya Afya ambapo bado changamoto ni nyingi jijini hapa pamoja na nchi nzima.

Aidha Meya Mwita amefarijika kuona hosipitali hiyo imewekeza katika vifaa tiba vya kisasa zaidi kuwemo nchini pamoja na uwepo wa Watanzania wengi katika eneo la utoaji huduma za viwango vya juu kabisa Tanzania.

Kwaupande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi za Huduma za Afya Aga Khan Kanda ya Afrika Mashariki Sulaiman Shahabuddin amemshukuru Meya Mwita kwa kutenga muda wake na kutembelea hospitali hiyo.

Amefafanua kuwa "ni faraja kwetu sana kukuona mahali hapa Mstahiki Meya ,Hospitali hii ni kwa ajili ya Wana Dar es Salaam na Watanzania wote, Ninacho mshukuru Mungu ni kuona hospitali hii sasa ikianza kuhudumia hata mataifa ya jirani kama Comoro, Zambia, Malawi, Msumbiji " amesema.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...