Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya kudhibiti UKIMWI (TACAIDS) Dkt. Leonard Maboko ametembelea mikoa ya Lindi na Mtwara kwa lengo la kufanya tathimini na ufuatiliaji wa utekelezaji wa shughuli za UKIMWI zinavyotekelezwa katika mikoa hiyo.

Akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Lindi Dkt. Mboko alisema kuwa kwa mujibu wa matokeo ya utafiti wa matokeo ya UKIMWI ya mwaka 2016/17 unaonesha maambukizi kwa mkoa wa Lindi yapo kwa asilimia 0.3 wakati kiwango cha kitaifa ni asilimia 4.7 kwa Tanzania bara.

Dkt. Maboko aliongeza kuwa hali hii haimaanishi kuwa kiwango cha maambikizi hakiwezi kuongezeka kwani ni wazi kabisa kuwa kuna fursa za kiuchumi ambazo zinaongezeka na kuongeza mwingiliano wa watu. 

Alishauri kuwa kinachotakiwa ni kuongeza jitihada katika kutoa Elimu ya kujikinga na maambukizi ya VVU pamoja na elimu ya mabadiliko ya Tabia.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe Godfrey Zambi alisema kuwa Mkoa wa Lindi bado unaendelea kutoa elimu kwa wananchi kwani uwezekano wa kuongezeka kwa kiwango cha maambukizi haupingiki.
Pichani kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya kudhibiti UKIMWI (TACAIDS) Dr Leonard Maboko

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...