Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo (kushoto) pamoja na mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Pwani ,Ramadhani Maneno, wakishiriki katika nguvu kazi ya ujenzi wa kituo cha afya Kirongwe wilayani Mafia ,wakati wa ziara ya kamati hiyo kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM kwa kipindi cha miaka miwili na nusu ya uongozi wa serikali ya awamu ya tano. Kuanza kwa ujenzi huo imetokana serikali kutoa kiasi cha sh. milioni 500 kwa ajili ya ujenzi huo ambao utakapokamilika kituo kitahudumia takribani wakazi kutoka vijiji vingi vinavyozunguka kata ya Kirongwe .(picha na Mwamvua Mwinyi).
Sehemu ya ujenzi wa mradi wa maji safi na salama ,(inayoonekana pichani),unaojengwa kijiji cha Jibondo ,wilayani Mafia,mkoani Pwani ,ambao utakapokamilika utakaogharimu karibia bilioni mbili .(picha na Mwamvua Mwinyi).
Mkuu wa Mkoa wa Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo akibeba ndoo ya samaki kumimina katika beseni la mama ambae anauza biashara ya samaki kwenye mwalo wa samaki wilayani Mafia.(picha na Mwamvua Mwinyi).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...