Na Editha Karlo,Kagera

MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoa wa Kagera umewahamasisha wakulima kupitia vyama vya ushirika na masoko kujiunga na mpango wa ushirika afya (AMCOS)katika maonesho ya nane nane Mkoani humu yalifonyika katika viwanja vya Kakyailabwa (AMCOS)Kujiunga na mpango wa ushirika afya viwanja Kyakailabwa.

Akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Maico Gaguti Meneja wa Mfuko wa bima ya afya Mkoa wa Kagera Elias Odhiambo alisema kuwa ushirika afya ni mpango maalum wa Bima ya afya kwa wakulima ambapo mpango huo utawawezesha wakulima kuchangia mara moja gharama za matibabu na kuwa na uhakika wa matibabu kwa mwaka mzima pale wanapougua.

Odhiambo alisema watakaojiunga na mpango huu watapata matibabu kwenye vituo vya tiba vilivyosajiliwa na mfuko nchi nzima ikiwa ni pamoja na huduma za kibingwa na vipimo.

Katika viwanja vya kyakailabwa kwenye maonyesho ya sikukuu ya nane nane banda la NHIF lilisheheni huduma mbali mbali ikiwa ni pamoja na upimaji afya bila malipo kwa magonjwa yasiyo ya kuambukiza, usajili wa Ushirika Afya,Toto Afya na Bima kwa wajasiliamali ambapo muitikio wa wananchi kujitokeza kupima afya zao ni mkubwa

Mkuu wa mkoa wa Kagera Brigedia Generali Marco Gaguti alitembelea banda la NHIF na kushiriki katika upimaji wa Afya pia alihaidi kuhamasisha wakulima kujiunga na mpango huo kwaninutawasaidia wakulima kuwa na uhakika wa matibabu pale wanapougua wao na familia zao.
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Maico Gaguti akipima afya kwenye banda la mfuko wa bima ya afya(NHIF)kwenye viwanja vya Kyakailabwa wakati wa sherehe za nane nane.
Meneja wa Bima ya afya Mkoa wa Kagera Elias Odhiambo akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Maico Gaguti juu ya mpango wa ushirika afya kwa wakulima
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Maico Gaguti akipata maelezo kutoka kwa mtumishi wa mfuko wa bima ya afya katika banda la NHIF baada ya kutembelea kwenye nane nane viwanja vya Kyakailabwa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...