Na Ripota Wetu,Globu ya jamii
ALIELYEKUWA Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja Vya Ndege Tanzania Richard Mayongela athibitishwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini.

Taarifa iliyotolewa leo kwa vyombo vya habar imesema kuwa amethibitishwa kwenye nafasi hiyo  na Kaimu Mkurugenzi wa Railimali na Utawala  Lawrance Thobias wakati wa Mkutano wa Mameneja wa viwanja vya mikoani na Wakuu wa Vitengo mbalimbali vya Mamlaka.

Amefafanua kwa kueleza kwamba  amethibitisha kupokea barua ya uthibitisho huo kutoka kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwele mara baada ya kuona Utendaji wake mzuri katika Mamlaka.

Hivyo kuanzia sasa Mayongela ndio Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka ya viwanja vya ndege nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja Vya Ndege Tanzania Richard Mayongela

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...