Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii .

SERIKALI ya Sierra Leone kupitia wizara Elimu na Ufundi na Elimu ya Juu umetembelea Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Nchini (HESLB) kujifunza na bodi hiyo inavyotoa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu .

Ujio huo umekaa kwa wiki moja katika bodi hiyo ikiwa ni kuangalia namna ya kuweza kujifunza na kwenda kuanzihsa chombo hicho nchini Sierra Leone.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi Mtendaji Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Nchini (HESLB) , Abdulzaq Badru amesema kuwa nchi sierra leone kufika hapo ni kutokana na umahiri katika uchakataji wa mikopo kwa wanafunzi kwa elimu ya juu.

Amesema kuwa ujumbe huo umepita katika nchi ya Ghana na kisha Tanzania kuangalia namna ya uendeshaji wa bodi katika utoaji wa mikopo.

Ujumbe huo uliongozwa na Naibu Waziri wa Elimu , Ufundi na Elimu ya Juu ya Nchini Sierra Leone Dkt. Turad Senesie , Naibu Katibu Mkuu Wizara fedha Mr. Matthew Dingie , Naibu Mkurugenzi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii na Bima Mohammed Gondoe na wajumbe wengine.

Naibu Waziri wa Elimu , Ufundi na Elimu ya Juu ya Nchini Sierra Leone Dkt. Turad Senesie amesema HESLB inafanya vizuri katika uchakataji wa mikopo na kusema kuwa wanatarajia kuanzisha chombo kama hicho nchini kwao.
Mkurugenzi Mtendaji Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Nchini (HESLB) , Abdulzaq Badru akizungumza na waandishi wa habari  (hawapo pichani) wakati wa kuwaaga ujumbe wa Sierra Leone waliotembelea bodi hiyo.
Naibu Waziri wa Elimu , Ufundi na Elimu ya Juu ya Nchini Sierra Leone Dkt. Turad Senesie akizungumza na waandishi habari kuhusiana na alichojifunza katika bodi ya mikopo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...