Katibu mtendaji Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU), Prof Cherles Kihampa akizungumza na waadishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuhusu tarehe ya mwisho ya kutuma maombi ya kujiunga na masomo katika vyuo vikuu mbalimbali hapa nchini, alisema Agost 15 mwaka huu itakuwa siku ya mwisho kutuma maombi hayo.
Na Chalila , Kibuda,Globu ya Jamii.

Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) imetangaza kufunga dirisha la awamu ya kwanza la maombi ya kujiunga na masomo ya shahada ya kwanza katika vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu hapa nchini.

Akizungumza na wanahabari makao makuu ya Tume hiyo jijini Dar es salaam, Prof. Charles Kihampa amesema kwamba dirisha hilo linafungwa leo Agost 15, na kufunguliwa kwa awamu ya pili septemba 3 mwaka huu.

Aidha Prof.Kahampa amewasisitiza waombaji wasome mwongozo wa programu zilizoidhinishwa kudahili pamoja na vigezo vya udahili vinavyotakiwa kwa kila programu ya masomo kabla ya kuanza kutuma maombi yoyote ya udahili.

Ikumbukwe kuwa dirisha la maombi ya elimu ya juu lilifunguliwa rasmi kwa awamu ya kwanza Julai 20, 2018.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...