Naibu Waziri wa Elimu ya Juu na Ufundi toka nchini Sierra Leone Dk. Turad Senesie (kulia) akiuliza swali kwa Kamishna Msaidizi wa Sera toka Wizara ya Fedha, Sauda Msemo (hayupo pichani) wakati Naibu Waziri huyo alipotembelea Ofisi za hazina na ujumbe wake ili kujifunza namna Wizara ya Fedha inavyoweza kutoa fedha kwa ajili ya Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu. Kushoto ni Wajumbe aliombatana nao toka nchini Sierra Leone.
 Kamishna Msaidizi wa Sera toka Wizara ya Fedha, Sauda Msemo (kulia) akifafanua jambo kwa ujumbe toka nchini Sierra Leone (hawapo pichani) uliokuja nchini kwa lengo la kujifunza namna ya uendeshaji wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu. Katikati ni Afisa Mawasiliano wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu, Omega Ngole na kushoto ni Msaidizi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi hiyo Godfrey Chawe.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha toka nchini Sierra Leone, Mathew Dingie (katikati) akiuliza swali kwa Kamishna Msaidizi wa Sera toka Wizara ya Fedha, Sauda Msemo (hayupo pichani) wakati walipotembelea Ofisi za hazina ili kujifunza namna Wizara ya Fedha inavyoweza kutoa fedha kwa ajili ya Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu. Kushoto ni Wajumbe aliombatana nao toka nchini Sierra Leone. Kulia ni Naibu Waziri wa Elimu ya Juu na Ufundi toka nchini Sierra Leone Dk. Turad Senesie.
 Afisa Msimamizi Mwandamizi wa Fedha toka Wizara ya Fedha,Alexander John (kushoto) akifafanua jambo kwa ujumbe toka nchini Sierra Leone uliokuja nchini kwa lengo la kujifunza namna Wizara ya Fedha inavyoweza kutoa fedha kwa ajili ya Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu.
Kamishna Msaidizi wa Sera toka Wizara ya Fedha, Sauda Msemo (kulia) akifafanua jambo kwa ujumbe toka nchini Sierra Leone uliokuja nchini kwa lengo la kujifunza namna Wizara ya Fedha inavyoweza kutoa fedha kwa ajili ya Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu.Picha na MAELEZO

 Kamishna Msaidizi wa Sera toka Wizara ya Fedha, Sauda Msemo (mwenye kilemba) akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe toka nchini Sierra Leone uliokuja nchini kwa ziara ya kikazi ya kujifunza namna ya uendeshaji wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...