Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) halijawahi kupata gawio kutokana na umiliki wa hisa 35 mtaji wa Star Media LTD tangu mwaka 2013 kwa sababu ya star Media kuripoti hasara ya sh.bilioni 61.

Akizungumza katika warsha ya Toleo Maalum kwa Wananchi na Kukusanya maoni kuhusu ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya mwaka 2016/2017 iliyofanyika Katika Ukumbi wa PPF Tower Mkaguzi wa Mashirika ya Umma Pascal Mahwago amesema kuwa star media iliripoti uchakavu wa vitu na kufanya TBC kukosa gawio licha ya kuwa na hisa.

Amesema kuwa ushauri wa CAG ulitaka kuhakikisha shughuli zote za kifedha zinafuatiliwa kwa ukaribu katika kuweza kupata gawio kutokana na uwekezaji wa hisa hizo.Kahwago amesema katika ukaguzi mwingine ni Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) lilikabidhi mali zisizohamishika kwa kampuni ya kufua umeme ya Songas mwaka 2004 zilizokuwa ndani ya Ubungo Complex kwa kupewa hisa 10,000 bila ya kukokotoa thamani halisi ya Mali walizokabidhi. 

Amesema Tanesco ilishauriwa kufanya tathimini na kupitia mkataba wa kuhamisha mali uliosainiwa ili kuangalia kama zilizohamishwa zinaendana na thamani ya hisa walizopewa.Aidha amesema kampuni ya Songs iliwekeza Euro 285.7 sawa na asilimia 73 katika mradi wa Songas hata hivyo hauonyeshi sehemu yeyote ya umiliki kwa serikali kwenye mradi huo licha ya uwekezaji mkubwa uliofanywa na serikali.

Kahwago amesema mapendekezo ya CAG ni serikali kupitia upya mpangilio wa mradi na kutathimini kama mkataba uliofanyika kwa kuangalia usawa wa pande zote mbili.
Kaimu Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Wendy Massoy akizungumza katika warsha ya Toleo Maalum kwa Wananchi iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Mkaguzi wa Nje wa Wizara Grace Trofumo akitoa mada kuhusiana na ukaguzi mbambali unaofanywa na CAG katika warsha iliyofanyika katika ukumbi wa PPF Tower jijini Dar es Salaam.
Mkaguzi wa Mashirika ya Umma Pascal Kahwago akizungumza kuhusiana na mada ya ukaguzi katika mashirika ya umma.
Mkaguzi wa Serikali za Mitaa Ally Said akitoa mada ya ukaguzi wa Serikali za Mitaa katika warsha ya Toleo Maalum kwa Wananchi na Kukusanya maoni kuhusu ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya mwaka 2016/2017 iliyofanyika Katika Ukumbi wa PPF Tower.
baadhi ya wadau katika warsha ya Toleo Maalum kwa Wananchi na Kukusanya maoni kuhusu ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya mwaka 2016/2017 iliyofanyika Katika Ukumbi wa PPF Tower
Picha ya pamoja ya wadau na mgeni rasmi Kaimu Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Wendy Massoy.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...