WANANCHI wilayani Serengeti mkoani Mara wametakiwa kijitokeza kwa wingi katika ujenzi wa  vibanda eneo la ujenzi wa Stendi mpya inayojengwa eneo la Stendi Kuu Mjini Mugumu baada ya stendi iliyokuwaikitumika kuwa finyu na miundombinu kuwa mibovu.

Ambapo hali hiyo  kusababisha mabasi makubwa kupaki nje ya stendi hiyo kinyume cha sheria.Hayo yamesemwa leo  na Mwenyekiti wa Halamshauri ya Wilaya ya Serengeti mkoani Mara Juma Porini  katika baraza la madiwani la mwaka.Amesema  kuwa mwitikio wa wananchi katika ujenzi wa vibanda hivyo umekuwa mdogo baada ya kutangaziwa mpaka sasa.

Hivyo Mwenyekiti ametumia fursa hiyo kuwatangazia tena wananchi kujitokeza kwa wingi kwani muda ambao ulitolewa kwa ajili ya kukamiliasha maombi umeisha.Lakini amesema  wameamua kuongeza muda kwa lengo la wananchi kijitokeza kwa wingi.“Mwitikio wa wananchi katika ujenzi wa vibanda hivi umekuwa mdogo licha ya kuwatangazia na bei ni nafuu kuchukua fomu ni Sh.50,000 tu, na akishajenga kibanda hicho atakitumia kwa muda wa miaka mitano.

"Katika kipindi hicho  akatakuwa anakitumia kwa kulipa 20,000 tu na baada ya miaka mitano kibanda kitarudishwa na ataanza kukitumia kwa kupangisha kulingana na mikataba itakavyosema” amesema Mwenyekiti.Aidha Mbunge wa Jimbo la Serengeti mkoani Mara Samson Ryoba(Chadema) anasema kuwa wanaendelea kujenga Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti bila kujali itikadi za vyama kwa lengo la kuletea wananchi Maendeleo.

Huku Katibu wa Madiwani Chadema Samson Wambura akitoa mapendekezo ya Chama hicho likiwemo suala la uboreshaji wa masoko katika Mjini Mugumu.Aidha Mkurugenzi wa Halmashaurti Juma Hamsini amesema kuwa tayari Halmashauri hiyo imeishaagiza taa za kufunga katika baadhi ya masoko ya jioni ili kuongeza ulinzi wa mali za wananchi.Pia ameahidi  kuendelea kutafuta wadau kwa lengo la kufunga taa za barabarani.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Juma Porini akisisitiza suala la wananchi kujitokeza kwa lengo la ujenzi wa vinanda eneo la Stendi Kuu ambapo kunajengwa stendi mpya ya Magari.
Madwani WilayaniSerengeti Mkoani Mara wakiwa katika baraza la Mwaka.
Mbunge wa Jimbo la Serengeti CHADEMA Samson Ryoba akisisitiza suala la Ushirikiano baina ya Madiwani wote bila kujali itikadi za vyka kwa lengo la kuletea wananchi Maendeleo.
Katibu wa Madiwani wanaoyokana na CHADEMA Wilaya ya Serengeti Samson Wambura akisoma hoja pendekezi za kamati ya chama hicho likiwemo suala la kuboresha Masoko katika Mji wa Mugumu.
Mkurugenzi wa Halamashauri ya Wilaya ya Serengeti Juma Hamsini akifafanua jambo kwa madiwani hao na kueleza jitiada za Halamashauri hiyo likiwemo suala la ununuzi wa taa za barabarani pamoja na Masoko ya jioni. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...