NA. GSENGOtV

Kukojoa mara kwa mara hasa nyakati za usiku, Kushindwa kuzuia mkojo, yaani ukichelewa kidogo unaweza kukutoka bila breki, Maumivu wakati wa kukojoa, Kuishiwa nguvu za kiume, Kupungua kwa uwingi wa mbegu (low sperm count), Maumivu wakati unafika kileleni, Damu kutokea kwenye mkojo au kwenye mbegu za kiume, Maumivu nyuma ya mgongo au hata nyonga nk basi uonapo dalili hizo unaweza kuanza kuhisi una saratani ya tezi dume.

Kupitia dalili hizo ni wazi kwamba afya ya mgonjwa itakuwa matatani kwenye mataabiko.Wahenga walironga mficha maradhi kifo humuumbua. Kila kiungo cha mwanadamu kikipata tatizo ni jukumu la matabibu kufanya uchunguzi na kutoa huduma kwa eneo lililodhurika, Haiingii akilini kwamba uendelee kuteseka ile hali tiba ipo. Nao wataalamu wanasema uchunguzi wa kutumia kidole hauhitaji gharama kubwa kama ilivyo njia nyingine za kutumia vifaa maalum vya uchunguzi.

Ni tamaduni tu za watu wenye mawazo machafu ndizo zinazo wafanya wengi kudhani kipimo cha kidole ni udhalilishaji, lakini madaktari waliosomea fani hiyo wanasema kuwa ni njia ya kawaida sana.Kwa kuliona hilo Hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini Mwanza imezindua hudumu za kliniki za muda wa jioni kwa siku za wikiendi na sikukuu, lengo likiwa ni kupanua wigo wa upatikanaji wa huduma za Afya kwa wananchi wote ambao watahitaji huduma za kibingwa muda wote.

Hasa wale ambao hawawezi kufika hospitali kutokana na kubanwa na kazi. Fuatilia kile kilichojiri katika uzinduzi ikiwa ni pamoja na mashuhuda wanaume wa Tezi dume.
Huduma za uchukuaji vipimo zikiendelea katika viwanja vya Hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini Mwanza 
Licha ya kuwa na idadi kubwa ya wahitaji wa kupima afya, idadi ya madaktari wahudumu wa afya iliendana na kasi. 
Meza na meza vitengo kwa vitengo katika Uzinduzi wa Huduma za Kliniki za Jioni za Bure Hospitali ya Rufaa Bugando jijini Mwanza. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...