Na Leandra Gabriel, blogu ya jamii

WANAWAKE wajasiliamali wapatao 400 Wilayani Mkuranga wamepewa mafunzo na kuku wa kufuga ili waweze kujikwamua kiuchumi na kuendeleza shughuli za kijasiriamali Wilayani humo.

Akiongea na vyombo vya habari Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Filberto Sanga ameeleza kuwa hadi kufikia mwakani akina mama wa Mkuranga watakuwa mbali sana kutokana na ufugaji huo wa kuku hao ambao watainua uchumi wa familia zao.Aidha amewataka akina Mama wa Wilaya ya Mkuranga kutumia mradi huo vizuri ili kuleta maendeleo kwani wamebahatika sana.

Naye Mkurugenzi wa Wilaya ya Mkuranga Mhandisi Mshamu Munde amesema kuwa kuku hao ni kwa ajili ya ufugaji katika kujikwamua kiuchumi na sio zawadi na amewataka akina mama hao kutumia ujuzi kuendeleza ufugaji na kuwaelimisha wengine kuhusiana na mafunzo hayo.

Pia ameeleza kuwa wajasiriamali hao wamepokea kuku 1058 kati ya kuku 4000 waliohaidiwa na akina Mama 100 wamepata kuku 10 kwa kila mmoja.

Mwenyekiti wa jukwaa la wanawake jukwaa la Wilayani Mkuranga bi. Mariam Ulega kuku 4000 ambao watagaiwa kwa akina mama 400 watagaiwa kwa wanawake wajasariamali waliohudhuria katika mafunzo hayo.Ameeleza kuwa kwa hicho kidogo wakitumie katika kuleta maendeleo yao binafsi na taifa kwa ujumla, amewataka wawe na ushirikiano ili waweze kufikia malengo yao.
Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga,Filberto Sanga akizungumza mbee ya Wanahabari (hawapo pichani),mapema leo kuhusu kupokea kuku kwa ajili ya Wajasiliamali Wanawake mkoa wa Pwani(Picha na Emmanuel Massaka Globu ya jamii)
Baadhi ya kuku waliopewa Wanawake wajasiliamai wilaya ya Mkuranga kwa ajili ya ufugaji
Baadhi ya Wanawae wa Wilaya ya Mkuranga wakiwahifadhi kuku wao katika matenga ya mbao,Wanawake 400 walipata kuku 10 kila mmoja kwa ajili wa mtaji wa kufuga kuku.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...