Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.Abdallah Ulega,amefungua rasmi maonesho ya Nane Nane kanda ya kati ambayo yanaenda sawa na Mashindano ya Nane ya Mifugo kitaifa yanayofanyika Jijini Dodoma.

Mhe.Ulega Amefungua Mashindano ya Mifugo ambayo yalianza mwaka 2011 na huwa yanafanyika Agosti 5 kila mwaka na hufanyika  Dodoma na hujumuisha Ng'ombe wa maziwa na nyama walioboreshwa pamoja na Mbuzi wa Asili.

Mhe.Ulega amesema kuwa lengo kuu la Mashindano hayo ni kutambua umuhimu na mchango wa rasmilimali za mifugo ya asili katika kuendeleza sekta ya mifugo nchini.

Aidha amesema kuwa zoezi hili linalenga kutambua juhudi na maarifa wanayotumia wafugaji wa mifugo ili kufuga kwa tija na hatimaye kuvutia wafugaji wengi na kuiga na kuingia kwenye ufugaji wenye tija kwa taifa.

Mhe.Ulega amesesisitaza kuwa Sekta ya Mifugo ni moja ya Sekta muhimu zinazochangia kupunguza umaskini wa wananchi na kukuza uchumi wa nchi kwani ni mhimili katika kuendeleza viwanda kama ilivyoainishwa katika mpango kabambe wa Mifugo Tanzania.

Hata hivyo Mhe.Ulega ametoa maagizo kwa wafugaji na wadau mbalimbali kuunda na kuimarisha vikundi na vyama vya ushiriki ili kuongeza kasi ya uwekezaji katika viwanda vya kusindika mazao ya mifugo na hatimaye kufikia malengo na kauli mbiu ya Nane Nane 2018 isomekayo ''WEKEZA''.

Aidha Mhe.Ulega ameagiza Halmashauri zote nchini kuhakikisha utekelezaji wa mfumo wa utoaji kinga mbalimbali za magonjwa ya mifugo uwe ni lazima kwa wafugaji wote nchi.

Kwa upande mwingine Mhe.Ulega amesema wafugaji pamoja na wafanya biasha  hawaruhusiwi kuhamisha au kusafirisha mifugo pamoja  mazao kutoka sehemu moja hadi nyingine bila kibali.

Hivyo imesababisha maeneo ya mipakani mwa nchi yetu imeshamiri biashara haramu za mifugo na mazao yake zisizo rasmi amewataka watendaji kusimamia sheria kwa kushirikiana na wadau ili kutatua changamoto ya utoroshaji wa rasilimali za mifugo yetu na mazao yake.Naibu Waziri wa Mifungo na Uvuvi,Abdallah Ulega   akizungumza na wananchi wa mkoa wa mkoa Dodoma wakati wa kufungua rasmi maonesho Nane Nane kanda ya kati na  mashindano ya nane ya Mifungo  kitaifa yanayo fanyika katika viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Mifungo na Uvuvi,Abdallah Ulega akiangalia viatu katika banda la  Magereza vinavyotegene  na ngozi katika maonesho ya Nane Nane Nane katika viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma.
 Naibu waziri wa Mifungo na Uvuvi,Abdallah Ulega akiwa ameambatana na Mkuu wa mkoa  wa Dodoma Dkt. Bilinith Mahenge wakitembelea banda la wajasiria mali katika maonesho ya Nane Nane yanayo fanyika  katika viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma.
 Naibu waziri wa Mifungo na Uvuvi,Abdallah Ulega  akiangalia samaki aina ya kamongo  alikaushwa  katika banda la  wajasiria mali katika maonesho ya Nane Nane yanayo fanyika  katika viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma.(Picha na Emmanuel Massaka Globu ya jamii)

 Wafungaji mbalimbali  wakionesha mifungo yao katika mashindano ya nane ya mifungo   yanayofanyika  kitaifa katika viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma(Picha na Emmanuel Massaka Globu ya jamii)
 Wafungaji mbalimbali  wakionesha mifungo yao katika mashindano ya nane ya mifungo   yanayofanyika  kitaifa katika viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma(Picha na Emmanuel Massaka Globu ya jamii)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...