Na Leandra Gabriel, blogu ya jamii
WAZIRI
wa Nishati Dkt.Medard Kalemani amefanya ziara katika Wilaya ya Mkuranga
katika kukagua utekelezaji wa utoaji wa huduma ya umeme kwa wananchi na
hakuridhishwa na utendaji wa baadhi ya wahusika katika idara hizo na
kuamua kuwaweka kando ili wenye kasi watekeleze jukumu hilo.
Katika
Ziara hiyo Kalemani amemuagiza meneja Tanesco mkoa wa Pwani
kumsimamisha kazi Mhandisi wa Mkoa na pia amemuagiza meneja wa wilaya
ya Mkuranga Mhandisi, Regina Mvungi kumsimamisha mhandisi mwenye dhamana
hiyo katika wilaya ya Mkuranga kwa kushindwa kufanya kazi ya kuwasha
umeme kwenye vijiji vilivyo kwenye mradi kata ya Vikundi.
Aidha
Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani ametoa siku 14 Wilayani Mkuranga
katika kuhakikisha umeme unawaka katika vijiji vyote vilivyokatika
mpango huo.Waziri hiyo aliyasema hayo Leo hii wakati wa ziara ya
kutembelea wilayani Mkuranga ili kuona namna ya upatikanaji wa huduma ya
Nishati ya Umeme katika Kata ya Kisiju,Vikindu na Tambani.
Kalemani
amesema kuwa mradi wa umeme vijijini (REA) awamu ya pili haikufanya
vizuri katika Tarafa ya Kisiju hivyo natoa siku 14 kuanzia kesho
kuhakikisha umeme unawaka, aidha Kalemani ametoa maagizo kwa viongozi
wa Tanesco katika ngazi ya Mkoa na Wilaya kuhakikisha umeme huo unawaka
kwa wakati.
Naye
Mbunge wa Mkuranga na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh Abdallah Ulega
amesema wananchi katika vijiji ambavyo vilitakiwa kupata umeme
walikata minazi na miembe yao ili kupisha miundo mbinu ya umeme lakini
ni zaidi ya miaka mitano tangu miundombinu ya umeme iwekwe na hakuna
umeme.
Aidha
Ulega amemshukuru Waziri Kalemani kwa ziara yake jimboni hapo kwani
anaamini italeta mabadiliko na amewataka watendaji waliopewa maagizo na
Waziri wayafanyie kazi mara moja.
Waziri
wa Nishati Dkt.Medard Kalemani(katikati)kwa kushiriki na viogizo
mbalimbali akikata utepe kuashiria uzinduzi wa umeme katika kijiji cha
Mkokozi Wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani.
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (alienyosha mkono) akizungumza na wanachi wa kata ya Kisiju wilaya ya Mkuranga ambapo amewaagiza watendaji wa Tanesco siku 14 wahakikishe umeme umewaka (Picha Emmanuel Massaka Globu ya jamii)
Wananchi wa Wilaya ya Mkuranga wakimsikiliza Waziri wa Nishati Dkt.Medard Kalemani.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...