Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Bulimba katika Kiwanja cha Mpira cha Victoria, Jimbo la Mwibara, wilayani Bunda, kabla ya Waziri huyo kugawa zawadi ya mshindi wa Bonanza la Kangi la mpira wa miguu ambapo timu ya mpira wa miguu ya Muungano pamoja na Miseni zote zinatoka Kata ya Butimba zilicheza. Lugola alitoa shilingi milioni 400 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya kidato cha tano na sita katika shule ya Sekondari Bulimba. 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola (kulia) akimuangalia Kapteni wa timu ya mpira wa miguu ya Muungano, Bwire Metwisele wakati alipokua anashangilia mara baada ya Waziri huyo kumkabidhi zawadi ya mshindi wa kwanza wa Bonanza la Kangi, kwa kuifunga timu ya Miseni magoli mawili bila. Timu zote zinatoka Kata ya Butimba wilayani Bunda, Mkoa wa Mara. Pia Lugola alitoa shilingi milioni 40 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya kidato cha tano na sita katika shule ya Sekondari Bulimba.
Mchezaji wa Timu ya Muungano ya Kata ya Butimba wilayani Bunda, Bwire Metwisele (kulia), akimdhibiti mchezaji wa timu ya Miseni, Jovin Andrew, katika mashindano ya Bonanza la Kangi lililofanyika katika kiwanja cha Victoria, Kijiji cha Bulimba. Timu ya Muungano iliifunga Miseni magoli mawili kwa bila.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola (kulia) akimsalimia mzee wa Kijiji cha Bulimba, Kata ya Butimba, Jimbo la Mwibara wilayani Bunda, wakati alipokua katika ziara ya kukagua mikradi ya maendeleo ndani ya Jimbo lake. Lugola pia alishiriki mashindano ya mpira wa miguu ya Bonanza la Kangi, iliyokutanisha timu mbili za Muungano na Miseni za Kata hiyo, Timu ya Muungano iliifunga Miseni magoli mawili bila. Pia katika hotuba yake, Mbunge huyo alitoa shilingi milioni 40 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya kidato cha tano na sita katika shule ya Sekondari Bulimba.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola (aliyeonyesha alama ya vidole) akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu za mpira wa miguu ya Muungano pamoja na Miseni pamoja na maafisa wa Wilaya ya Bunda, kabla ya kuanza kucheza katika kiwanja cha Victoria kijijini Bulimba, Jimboni humo. Lugola alitoa zawadi ya mshindi wa mashindano hayo na pia alitoa shilingi milioni 40 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya kidato cha tano na sita katika shule ya Sekondari Bulimba. Watatu kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Lydia Bupilipili. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...