Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii Tanga

Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango amewataka wakazi wa mkoa wa Tanga kutumia fursa ya uwepo wa Amana Benki katika mkoa huo kama fursa ya kujipatia Maendeleo kutokana na benki hiyo kuwa na huduma ya mikopo isiyokuwa na riba.

Waziri Mpango amesema hayo mkoani Tanga wakati alipokuwa akimwakilisha Waziri Mkuu Kassim Majaliwa katika uzinduzi wa tawi jipya la benki hiyo katika mkoa huo."nimefurahishwa na jitihada za Amana Bank katika kutanua huduma zake kwa wananchi wa mikoani. Vilevile, nimewasisitiza wana Tanga kutumia fursa waliyopata kutoka Amana Bank kwa kuwafikishia huduma za bank hiyo kwao,ikiwemo mikopo bila riba jambo ambalo litawasaidia sana kujiinua kichumi kwa kukopa na kurejesha kwa wakati"amesema Waziri Mpango.

Akizungumza kwa niaba ya benki hiyo Mkurugenzi wa Amana Benki Dk Muhsin Masoud, amesema Benki ya Kiislamu ya Amana hapa nchini imefungua tawi lake jipya jijini Tanga ikiwa ni sehemu ya mikakati ya Benki hiyo kufikisha huduma zake kwa watu wa mikoani.mesema kuwa Benki hiyo inatarajia kufungua matawi yake mengine Zanzibar na Dodoma hivi karibuni hili kuzidi kuwasogelea wananchi nakutaja kuwa akaunti zinazopatikana katika Benki hiyo, ni akaunti ya akiba ya wanafunzi, akaunti ya akiba ya Hijja, akaunti ya akiba ya mtoto(nuru), akaunti ya akiba ya mwanamke(anisaa) na akaunti binafsi.

ametaja kuwa kwa sasa Benki hiyo ya Amana inafikisha jumla ya matawi 8, matano yakiwa Dar es Salaam, Moja Mwanza,Arusha na hilo la jijini Tanga. Amana Benki ilianzishwa mnamo Novemba 24, 2011 kwa lengo la kukidhi haja ya wateja wa kibenki nchini ya kupata huduma zinazozingatia misingi ya sharia za Kiislamu.
Waziri wa Fedha na Mipango Philip Mpango akiwa na Mkuu wa Mkoa Wa Tanga , Martin Shigela wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa Tawi Jipya la Amana Benki Mkoani Tanga.
Waziri wa Fedha na Mipango Philip Mpango akifunua kitambaa cha jiwe la Msingi wakati wa uzinduzi wa tawi jipya la Amana Benki Mkoani Tanga
Mkuu wa Mkoa wa Tanga , Martin Shigela akizungumza wakati wa uzinduzi wa Tawi jipya la Amana Benki katika mkoa wake
Dk Muhsin Masoud,Mkurugenzi wa Amana Bank akielezea huduma zitakazotolewa katika tawi hilo la Mkoa wa Tanga.
Waziri wa Fedha Philip Mpango akiwa katika picha ya Pamoja na baadhi ya wateja mashuhuri wa benki hiyo wa mkoa wa Tanga.
Waziri wa Fedha akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi wa mkoa wa Tanga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...