Bweni la wavulana Shule ya msingi Giti iliyopo Wilayani Same limeteketea kwa moto baada ya moto kuunguza bweni pamoja na vitu vyote vilivyokuwemo ndani. 

Wanafunzi wote wamenusurika na moto huo, kwani moto uliwaka majira ya saa 2.00 usiku wanafunzi wakiwa katika vipindi vya usiku darasani.Wanafunzi wamepoteza kila kitu na kuhitaji msaada wa haraka ili kurudisha maisha yao katika hali ya kawaida. 

Mkuu wa Wilaya ya Same,Mh  DC Same Rosemary Senyamule  akiwa ameambatana na Kamati ya ulinzi na usalama pamoja na Afisa elimu ,walitembelea eneo la tukio na kuona uhitaji wa marakebisho ya haraka kwa jengo linalotegemea kuhamishia wanafunzi hao ili waendelee na masomo. 

DC Rosemary amewataka Wataalamu wa zimamoto na wakaguzi wa shule kufanya kaguzi za mara kwa mara katika taasisi zote ili kuchukua tahadhari za matukio kabla hayajatolea. 

Naye Mwenyekiti wa Conference kanda ya kaskazini Mch. Ijiko (kanisa la SDA) ambao ndiyo wamiliki wa shule hiyo amewaomba wadau kushirikiana nao ili kurudisha bweni hilo katika hali ya kawaida na kuwawezesha wanafunzi kurudishia mazingira bora ya kusomea.

Tukio hilo litokea Julai 29,2018 kata ya Mamba myamba Wilayani Same.
 DC Same Rosemary Senyamule (wa tatu kulia) akiwa ameambatana na Kamati ya ulinzi na usalama pamoja na Afisa elimu wakiwa katika kikao cha pamoja mara baada kutembelea eneo la tukio na kuona uhitaji wa marakebisho ya haraka kwa jengo linalotegemea kuhamishia wanafunzi hao ili waendelee na masomo. 
Muonekano wa Bweni la wavulana Shule ya msingi Giti iliyopo Wilayani Same lilivyotekea kwa moto baada ya moto kuunguza bweni pamoja na vitu vyote vilivyokuwemo ndani. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...