NA IS-HAKA, ZANZIBAR.

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Dk.Bashiru Ally amesema CCM inaendelea kuimarika na hakuna Chama chochote cha kisiasa nchini kinachoweza kushindana nacho katika uringo wa siasa za ushindani wa sera za maendeleo kwa wananchi wa makundi yote.

Kauli hiyo aliitoa mara baada ya kuwasili kisiwani Pemba katika mwendelezo wa ziara yake ya kujitambulisha ambapo amezungumza na wanachama mbalimbali katika ukumbi wa Skuli ya Sekondari ya Fidel Castro Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Alisema kutokana na uimara huo hakuna chama kingine mbadala wa Chama Cha Mapinduzi kinachoweza kushuka kwa wananchi nyumba kwa nyumba na kuratibu kero zao kisha kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu.

Dk.Bashiru aliwahakikishia wanachama na viuongozi hao kuwa CCM bado ipo imara na itapata ushindi wa kihistoria mwaka 2020 kwa nchini nzima kuliko ushindi unaopatikana kwa sasa katika uchaguzi mdogo unaoendelea katika maeneo mbalimbali nchini.
 KATIBU Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru Ally Akizungumza na wanachama na viongozi wa CCM wa Mikoa miwili ya Pemba katika ukumbi wa skuli ya Fidel Castro.
 Mwenyekiti wa CCM  Mkoa wa Kaskazini Pemba Ndugu Mberwa Hamad Mberwa akimpa tia Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru zawadi ya ndizi ya mkono wa Tembo.
  KATIBU Mkuu wa CCM Tanzania Dk.Bashiru Ally akitembea kuelekea ofisi ndogo ya CCM Chake chake mjini Pemba.
Katibu Mkuu wa CCM Tanzania akisalimiana na mwanachama mpya kutoka chama cha CUF aliyejiunga na CCM Amina Juma Nassoro

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...