Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Richard Mayongella  amewataka abiria wanaotumia viwanja vya ndege kusafiri maeneo mbalimbali kuacha kukimbilia kwenye mitandao pindi wanapobaini kuna upotevu wa vitu.

Amewataka kutumia mamlaka husika  katika uwanja huo ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa kamili ya jambo linalolalamikiwa.

Mayongella ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kusambaa kwa taarifa ya abiria aliyotumia uwanja wa ndege wa Dar es Salaam kudai ameibiwa wakati ukaguzi wa mwisho

Amesema katika viwanja vya ndege kuna vitengo mbalimbali ikiwemo kituo cha polisi, hivyo kama kuna abiria anaibiwa mizigo au chochote basi ni vema kuripoti kwanza kwenye vyombo hivyo ili kuruhusu kufunguliwa jarada la uchunguzi na si kwenye mitandao ya kijamii na kuchafua taswira ya nchi.

Mayongella amesema kuwa abiria huyo alikuwa anasafiri kuelekea ughaibuni  nakudai kuibiwa pochi yake katika Uwanja cha Ndege wa Kimataifa cha Julius  Nyerere.

 Alikiri kuwa Septemba 8 mwaka huu abiria huyo jina wanalihifadhi alikuwa anasafiri na ndege aina Emirates lakini wakati anafanya taratibu za kufanyiwa ukaguzi na kumalizika baadae akaja nakudai ameibiwa pochi.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Richard Mayongela (katikati)  akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na shutuma za wizi wa pochi kwenye ukumbi wa mikutano wa Jengo la Pili la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TBII).
Bw. Wael Hassan (kulia) akiushukuru uongozi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kwa kuonesha picha zilizopigwa na kamera za Usalama za tukio la kulalamikiwa kwa wizi wa pochi ya dada yake (jina limehifadhiwa), aliyesafiri tarehe 8 Septemba, 2018 akielekea Dubai. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...