NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani[CCM akizungumza katika mkutano wa hadhara eneo sokoni wilayani Pangani kabla ya kushuhudia utiliaji wa saini ya mkataba wa maji kutiliana saini mkataba wa utekelezaji wa mradi huo baina ya Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Tanga-Uwasa) wilayani hapo.
 MKUU wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah akizungumza katika mkutano huo kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella kushoto ni Katibu tawala wa wilaya ya Pangani Mwalimu Hassan Nyange.
 MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigel,a katika akiwa na Mkuu wa wilaya ya Pangani  Zainabu Issa wakifuatilia mkutano huo kulia ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Pangani Hamisi Mnegero akifuatiwa na Naibu WAziri wa Maji na Umwagiliaji ambaye pia ni mbunge wa Jimbo la Pangani CCM Jumaa Aweso


NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso amemtaka mkandarasi toka Kampuni ya Macarious Hotela and Co.Ltd ya Jijini Tanga kumaliza mradi wa maji katika mji wa Pangani wenye thamani ya zaidi ya Shilingi milioni 500 kwa wakati kabla ili kuweza kutoa fursa kwa wananchi kunufaika na huduma hiyo muhimu.

Aweso ambae pia ni Mbunge wa Pangani ameyasema hayo wakati wa zoezi la kutiliana saini mkataba wa utekelezaji wa mradi huo baina ya Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Tanga-Uwasa) Wilayani hapo.

“kwa kweli hatuta kuwa na msamaha kwa Mkandarasi atakae kwenda kinyume na matakwa ya utekelezaji wa mradi huu kama yalivyoainishwa katika mkataba tutakuwa wakali kweli”Alisema Aweso.

Aidha alisema mradi huo utawanufaisha wananchi wa Pangani Mashariki na Magharibi ambapo unatarajiwa kutekelezwa ndani ya kipindi cha miezi kumi kama makubaliano yalivyoafikwiwa na pande mbili upande wa Serikali na Mkandarasi.

Alisema Wizara hiyo ya Maji na Umwagiliaji imetenga fedha hizo ili kutatua kero za wananchi wa maeneo hayo hivyo Serikali haitakuwa na uvumilivu na mkandarasi atakae kwamisha jitihada hizo za Serikali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...