Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
MKUU wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo amepokea kiasi cha Shilingi Milioni Tano (5,000,000) kutoka kwa uongozi wa Azam Media wakichangia katika kampeni ya Tokomeza Zero.
Akizungumza mbele ya waandishi wa habari, Afisa Mtendaji Mkuu wa Azam Media Tdo Mhando amesema kuwa wanaunga mkono jitihada zinazofanywa na Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe ya kuhamasisha wananchi kuchangia ili kutokomeza Zero kwenye Wilaya hiyo.
Tido amesema kuwa, wao kama uongozi wa Azam wanachangia kiasi ch Milioni tano (5,000,000) ili kusaidia kampeni hiyo na bado wataendelea kushirikiana katika nyanja zingine za kimaendeleo kwani huu ni mwanzo.

Baada ya kupokea hundi ya Kiasi hicho, Mkuu wa Wilaya Jokate amewashukuru uongozi wa Azam kwa kuweza kuona umhimu wa kuungana nae kwa kushirikiana  na kumpatia kiasi hicho kitakachowasaidia kuhakikisha wanafunzi wanapata mahitaji yote kwenye kipindi hiki kuelekea mtihani wa kidato cha nne.
Jokate amesema wanafunzi wanahitaji msaada mkubwa kutoka kwa wananchi mbalimbali kwa kiasi chochote walichonacho ikiwemo mahitaji muhimu kama unga, sabuni, mafuta na kadhalika, kwani katika kipindi hiki wapo wamekaa mahali wanajisomea na vitu vinavyopatikana vinawasaidia wao.
Amesema kwua, wanafunzi hao kwa sasa wanahudumiwa na serikali ya Wilaya ya Kisarawe  chini ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Twala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ambaye ni Mbunge  wa Kisarawe Seleimani Jaffo.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Azam Media Tido Mhando akimkabidhi mfano wa hundi ya Shilingi Milioni tano (5,000,000) kwa Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo kwa ajili ya kampeni ya Tokomeza Zero.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...