*Yaonya wanaozichezea ,yataka ziheshimiwe na kila mmoja wetu
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
BENKI Kuu ya Tanzania(BoT) imewataka Watanzania wote kuhakikisha wanatunza fedha zetu kwani ni mojawapo ya tunu na alama muhimu ya uchumi wa nchi yetu.
Pia fedha ni alama ambayo inapaswa kuheshimwa kama zilivyo alama nyingine kwa mfano Bendera ya Taifa.
Taarifa ya BoT kwa vyombo vya habar ambayo wameitoa leo inasema utunzaji mzuri wa fedha zetu utapunguza uwezekano wa fedha hizo kuchakaa mapema na kupunguza gharama za uchapishaji."Kwa
mujibu wa Sheria ya Benki Kuu ya Tanzania ya mwaka 2006, kifungu cha
26, BoT ndiyo taasisi pekee yenye mamlaka ya kutoa noti na sarafu katika
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania," imesema taarifa hiyo.
Pia imesema noti na sarafu hizo zina alama muhimu inayolitambulisha taifa la Tanzania ambayo ni nembo ya Bwana na Bibi. Imefafanua alama hiyo inapaswa kuheshimwa kama zilivyo alama nyingine kwamfano Bendera
ya Taifa.
Pia noti na sarafu zote zimetengenezwa kutoa thamani ya kisheria (legal
tender) kama ilivyoandikwa juu ya noti au sarafu husika na pia Benki Kuu pekee ndiyo yenye mamlaka ya kuharibu noti na sarafu.
Taarifa hiyo imefafanua kuhusu hilo kupitia kifungu cha 28 kikisomwa pamoja na kifungu cha 30 cha Sheria ya Benki Kuu ya Tanzania ya mwaka 2006."Benki Kuu inatoa rai kwa wananchi kuzitunza fedha zetu kwa kuwa ni mojawapo ya tunu na alama muhimu ya uchumi wa nchi yetu.
"Vilevile, utunzaji mzuri wa fedha zetu utapunguza uwezekano wa fedha hizo kuchakaa mapema na kupunguza gharama za uchapishaji," imesema taarifa hiyo ya BoT.Imesisitiza kwa mujibu wa Sheria ya Benki Kuu ya Tanzania ya mwaka 2006, kifungu cha 26, Benki Kuu ya Tanzania ndiyo taasisi pekee yenye mamlaka ya kutoa noti na sarafu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Pamoja na mambo mengine imesisitiza umuhimu wa alama hiyo inapaswa kuheshimwa kama zilivyo alama nyingine kwamfano Bendera ya Taifa. Na kwamba Noti na sarafu zote zimetengenezwa kutoa thamani ya kisheria (legal tender) kama ilivyoandikwa juu ya noti au sarafu husika.
"Na pia Benki Kuu pekee ndiyo yenye mamlaka ya kuharibu noti na sarafu (kifungu cha 28 kikisomwa pamoja na kifungu cha 30 cha Sheria ya Benki Kuu ya Tanzania ya mwaka 2006) ," amesema.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...