MKAZI wa Kigamboni, jijini Dar es Salaam, Salum Juma, ameibuka kidedea baada ya kukabidhiwa Sh Milioni 5 kutoka kampuni ya michezo ya kubashiri matokeo ya bikosports, baada ya mdau huyo wa michezo ya kubahatisha kutabiri michezo 11 ya mpira wa miguu duniani, jambo lililowavutia Bikosports na kuamua kumpa bonasi kama sehemu ya kuwajali wachezaji wa bahati nasibu yao.

Akizungumza katika Mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Msemaji wa Biko sports, Jeff Lea alisema kitendo cha shabiki huyo kubashiri michezo 11 kimewafanya waone haja ya kumpa bonasi, akiamini kuwa haitawavunja nguvu wasahiriki wao badala yake itawapa mwamko katika kushiriki mbio za kuwania Sh Milioni 97 kwa mtu atakayeibuka shujaa wa kubashiri michezo 13 kama droo yao kubwa inavyotaka.

Leya alisema licha ya wadau mbalimbali kuendelea kuvuna fedha mbalimbali kwa kubashiri na Kampuni yao ambayo namba ya kampuni ni 101010, ambapo mchezo huo unaweza kuchezwa kwa kutuma jamvi kwa *149*89# bila kusahau kwa kuingia kwenye mtandao wao moja kwa moja kujionea mpangilio mzima wa mchezo wao unaoweza kuchezwa bila kuwa na akaunti huku ushindi ukipatikana moja kwa moja kwenye simu ya mkononi.

“Biko Sports tunawajali sana wateja wetu ndio maana leo tumeamua kwa dhati kabisa kumpa bonasi ya Sh Milioni tano ndugu yetu Juma kwa sababu amejitahidi kwa kubashiri michezo 11, akishindwa miwili tu ili avune Sh Milioni 97 kutoka kwetu, ambapo bikosports ina machaguo Zaidi ya 125.

“Biko Sports ni rahisi kubashiri na kushinda bila kusahau jinsi tunavyojali wateja, hivyo kwa pamoja tunaamini watanzania wataendelea kubashiri kwakupitia kampuni yetu kwa sababu tumeboresha mno huduma zetu na fedha zetu zinalipwa muda mfupi tu baada ya kufanikiwa kushinda kwenye jamvi husika,” Alisema.

Msemaji wa BIKOSPORTS Tanzania, Jeff Lea kulia, akikabidhi hundi ya sh Milioni 5 kwa mshiriki wa bahati nasibu ya kubashiri matokeo ya michezo ya mpira wa miguu, Salum Juma wa pili kutoa kulia, aliyepewa bonasi ya kiasi hicho baada ya kubashiri mechi 11 badala ya 13 ambayo ndio droo kubwa ya sh milioni 97 hali iliyowavutia biko sports kumpa bonasi hiyo kama sehemu ya kuwajali wateja wao. Wengine ni Maulid Kitenge Balozi wa Bikosports pamoja na Mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Chiku Saleh wakati kushoto kwake ni Meneja Uendeshaji wa Bikosports Tanzania Lucas Kiangi. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...