Chama cha Mapinduzi(CCM) leo kimehitimisha kampeni zake za ubunge jimbo la Monduli kwa aina yake kutokana na wapambanaji wake kujipanga vyema katika kubwaga sera wakimnadi mgombea wa chama hicho Julius Kalanga.

Kampeni hizo zimefurika mamia ya wakazi wa jimbo hilo katika eneo la Mto wa Mbu na zimefungwa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM bara Rodrick Mpogoro na mgeni mashuhuri Selemani Jafo ambaye ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI).

Timu ya wapambanaji wengine iliyokuwa kwenye kampeni hizo kwa siku zote iliongozwa na William Ole Nasha, pamoja na timu ya wabunge mahiri Joseph Msukuma, Sixtus Mapunda, Catherine Magige, Ester Mahawe, Venanse Mwamoto, Dk. Kiluswa, Mariam Ditopile, Matha Mlata, Dk. Godwin Mollel, Anna Lupembe, Edwin Sanda, Godluck Mlinga, Jitu Son, Fratei Massey, na viongozi wengine wa Jumuiya zote za CCM Taifa.

Wapambanaji hao wamewaomba wananchi wa jimbo hilo kumchagua mgombea huyo kuwa Mbunge wao ili aweze kutatua vyema kero zinazowakabili kwa kushirikiana vyema na wabunge wengine huku wakiahidi kumsaidia kuwasilisha bungeni kero za watu wa Monduli ili zitatuliwe na serikali.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM bara Rodrick Mpogoro akiwa na viongozi wengine katika ufungaji wa kampeni za ubunge jimbo la Monduli.

Mbunge wa Kisarawe na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI)Selemani Jafo akizungumza katika ufungaji wa kampeni za ubunge jimbo la Monduli.

Wananchi waliohudhuria kampeni za ubunge za CCM jimbo la Monduli
Wananchi waliohudhuria kampeni za ubunge za CCM jimbo la Monduli

Wananchi waliohudhuria kampeni za ubunge za CCM jimbo la Monduli

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...