VICTOR MASANGU,KISARAWE 

WADAU mbali mbali wa maendeleo hapa nchini katika kuunga juhudi za Rais wa awamu ya tano Dk John Pombe Magufuli katika kuboresha sekta ya elimu wamempongeza na kumuunga mkono mkuu mpya wa wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo kwa kuweza kuanzisha kampeni maalumu kwa ajili kutokomeza ziro kwa wanafunzi wa shule za sekondari kwa lengo la kuweza kuongeza kasi ya kiwango cha ufaulu.

Pongezi hizo wamezitoa wakati wa halfa fupi ambayo iliandaliwa na mkuu huyo wa wilaya kwa lengo la kuweza kuchangia fedha katika sekta ya elimu ambazo zitaweza kuwa mkombozi mkumbwa katika kuwasaidia wanafunzi kuweza kufanya vizuri katika masomo yao husaani pindi wanapomaliza katika kidato cha nne.

Wakizungumza katika hafla fupi ya uchangiaji wadau wa maendeleo akiwemo Mohameda Kilumbi ambaye pia ni diwani wa wa kata ya Kibuta pamoja na Hamisa Mobeto wamesema kwamba wameamua kuchangia kwa hali na mali katika sekta ya elimu kwa lengo la kuweza kuborsha sekta ya elimu kwa wanafunzi ambao wamekuwa wakifanya vibaya katika mitihani yao.

“Kwa kweli sisi kama wadau wa maendeleo tumeona umhumimu wa kushiriki katikam zoezi hili la kumuunga juhudi za serikali ya awamu ya tano katika kuchangia sektaya elimu, na pia kwa pamoja tumeungana kumuunga mkono mkuu wa wilaya wetu ambaye ameteuliwa hivi karibuni lakini lengo letu kubwa ni kuhusina na hii kampeni ya kutokomeza Ziro katika wilaya ya Kisarawe,”waliwema wadau hao.
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokete Mwegelo akizungumza jambo wakati wa halfa iliyoandaliwa kwa ajili ya uchagiaji katika sekta ya elimu yenye lengo la kutokomeza ziro kwa wanafunzi wa shule za sekondari. 
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo akiwa na na wadau mbali mbali wa maendeleo katika halfa hiyo iliyofanyika katika shule ya Sekondari Minakaki. 
Diwani wa kata ya Kibuta Mohamed Kilumbi akizungumza jambo wakati wa halfa hiyo ya uchangiaji kwa ajili ya kutokomeza ziri katika halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe .PICHA NA VICTOR MASANGU .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...