Mkuu wa wilaya ya Arumeru Mh. Jerry Muro ameendelea kutatua kero na changamoto zinazowakabili wananchi wa Wilaya ya Arumeru ikiwemo kero sugu ya changamoto ya migogoro ya ardhi.

Dc Muro kupitia mkakati wake wa kutatua kero za wananchi ( PAPO KWA PAPO ) amefanikiwa kutatua kero ya utapeli wa kuuziwa viwanja vyenye migogogoro kwa kuamuru baadhi ya wamiliki wa makampuni yanayojishughulisha na biashara ya viwanja ( REAL ESTATE ) kurudisha fedha za wananchi waliouziwa viwanja vyenye matatizo ndani ya mwezi mmoja.

Aidha Dc Muro amezipiga marufuku kampuni zoote zinazojihisisha na udalali wa viwanja kutokufanya kazi katika Wilaya ya Arumeru mpaka hapo watakapopata maelekezo rasmi kutoka katika Ofisini ya Mkuu wa Wilaya lengo likiwa ni kukabiliana na ongezeko la uuzwaji wa ardhi za vijiji pasipo kufuata taratibu.

DC Muro anaendelea na zoezi lake lakushughulikia kero za Wananchi kwa mtindo wa PAPO KWA PAPO.
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Mh. Jerry Muro akizungumza na na baadhi ya wamiliki wa makampuni yanayojishughulisha na biashara ya viwanja ( REAL ESTATE ),ambapo amezisimamisha kampuni hizo kufanya shughuli hiyo na kuwata kurudisha fedha za wananchi waliouziwa viwanja vyenye matatizo ndani ya mwezi mmoja. 
Baadhi ya Wakazi wa Arumeru wakimsikiliza Mkuu wa wilaya hiyo ya Arumeru Mh. Jerry Muro alipokuwa akizungumza nao kuhusu kero na changamoto mbalimbali walizonazo,kuhakikisha zinapatiwa ufumbuzi na majibu ya papo kwa papo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...