WILAYA ya Namtumbo mkoani Ruvuma kupitia Mkuu wake wa Wilaya Sophia Mfaume Kizigo imesaini mkataba wa lishe bora, ambapo wamedhamiria malengo, vipaumbele na majukumu yote wanayotakiwa kuyatimiza yanatimia.

Akizungumza baada ya kusaini mkataba huo Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo, Kizigo amesema mkataba huo ni wa miaka 4 (2018 hadi 2021).

Amefafanua kwamba licha ya kwamba Ruvuma ni mkoa unaozalisha chakula kwa wingi sana na kulisha taifa lakini Ruvuma hiyohiyo ipo katika mikoa 5 ambayo ina hali mbaya sana ya lishe bora.

"Ruvuma kama mkoa kuna udumavu (stunting) asilimia 44, utapiamlo mkali asilimia 2.6, uzito pungufu asilimia 13.7, Upungufu wa damu (anaemia) na uzito mkubwa asilimia 21.1," amefafanua.

Pia ameongeza mkataba huo unaelekeza mpango mkakati wa lishe bora, kutoa elimu kwa wananchi ili wabadili tabia katika ulaji unaofaa, elimu ya lishe kwa jamii na mkakati wa kutengeneza chakula dawa.

Mkuu huyo wa Wilaya ameelezea namna ambavyo mkataba huo ukisimamiwa vema utakavyoleta mabadiliko kwa kufanikisha Wilaya ya Namtumbo inafanikiwa katika suala la lishe bora. 
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe. Christina Mndeme akiimkabidhi Mkuu wa Wilaya Sophia Mfaume Kizigo mkataba wa kufanikisha lishe bora kwa Wananchi mapema jana,mkoani humo
Pichani kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Sophia Mfaume Kizigo ikisaini mkataba wa lishe bora kwa Wananchi,kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma,katika mkataba huo Wialaya ya Namtumbo wamedhamiria malengo, vipaumbele na majukumu yote wanayotakiwa kuyatimiza yanatimia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...