MKUU wa wilaya ya Pangani Mkoani Tanga Mhe. Zainabu Abdallah ameagiza vyombo vya ulinzi na usalama wilayani humo kufanya uchunguzi wa kina ufanyike ili kuweza kubainika sababu za mauaji ya dereva wa bodaboda Mohamed Ally alimaarufu kama Sharo aliyekuwa anafanya kazi zake Pangani mjini.  
Inadaiwa mauaji ya bodaboda huyo yalitokea jioni ya Septemba 22 mwaka huu na mwili wake kupatikana Jumapili na kuzikwa juzi mara baada ya kukodiwa na watu wasiojulikana ambao walitaka awapeleka Tanga mjini na walipofika njiani wakatekeleza mauaji hayo kwa kumnyonga hadi umauti ulipomkuta na kuchukua pikipiki yake kutokomea kusikojulikana. 
Akizungumza mara baada ya kuitembelea familia ya marehemu na kutoa pole, Mkuu huyo wa wilaya alisema wamepokea kwa masikitiko makubwa na mshtuko wizi huo na mauaji hayo ya bodaboda ambaye ni kijana mjasiriamali. 
 “Kijana huyu mkazi wa Pangani ameuwawa kikatili sana kwa kunyongwa na watu wasiokuwa na utu na kuchukua pikipiki aliokuwa akifanyia biashara ….inaumiza kijana asie na hatia anayejitafutia riziki kujikwamua kimaisha ndoto zake zinakwamishwa”,alisema. 
 Aidha alisema wanalaani vikali vitendo hivyo huku akiviagiza vyombo husika kufanya uchunguzi wa tukio hilo haraka ili wahusika waweze kuchukuliwa hatua kwa kupelekwa kwenye vyombo vya kisheria. 
DC ZAinab alisema wanatarajia kukutana na kuongea na chama cha waendesha BodaBoda wilaya ya humo kuhusu jambo hili na mustakabali wao hasa kwenye masuala ya ulinzi na usalama.
 MKUU wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah kulia akimfariji mama wa dereva wa bodaboda aliyeuwawa Mohamed Ally alimaarufu Sharo anayefanya kazi zake Pangani mjini ambaye inadaiwa alikodisha na watu wasiojulikana na kufanya mauaji hayo
 MKUU wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah kushoto akimpa pole mama wa bodaboda aliyeuwawa Mohamed Ally alimaarufu Sharo anayefanya kazi zake Pangani mjini ambaye inadaiwa alikodisha na watu
wasiojulikana na kufanya mauaji hayo
 MKUU wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah katikati akiteta jambo na ndugu wa marehemu kushoto ni Katibu Tawala wa wilaya ya Pangani Mwalimu Nyange Hassani katikati ni Afisa Tawala wa wilaya hiyo Gipson

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...