Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

MKUU wa Wilaya ya Namtumbo, Sophia Mfaume Kizigo ametoa ufafanuzi kuhusu ziara ambayo ameifanya katika wilaya zote za wilayani humo huku akieleza namna ambavyo imesaidia kusikia changamoto za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Wilaya huyo ni kwamba ziara hiyo  ilikua na malengo makubwa matatu  ambayo yalitofautiana kulingana na kata husika. Akizungumzia ziara hiyo leo amesema utofauti ulikuja kwasababu kuna kata ambazo alikuwa tayari  ameshazitembelea, hivyo ziara hiyo ilikua wakimpokea kwa mara ya pili.

Wakati kwa Kata zingine alikuwa akipokelewa kwa mara ya kwanza.Ametaja malengo ya  yake  ya ziara hiyo ni kwamba kwa kata ambazo ziara hiyo ni kwa mara ya kwanza,lengo namba moja ilikuwa kujitambulisha. Pia kuhamasisha uhifadhi huku akifafanua alikuwa ameambatana na  wakuu wa idara muhimu kama kilimo, ardhi, ufugaji na uvuvi, misitu, sheria,sanaa utamaduni na michezo pamoja na kamati yote ya ulinzi na usalama ya wilaya.

Wakuu wa idara za kilimo, ardhi, mifugo na OCD walipata nafasi ya kutoa somo fupi kuhusu uhifadhi. Kila mtaalamu kwa kitengo chake alieleza njia bora zaidi za kufanya shughuli mbalimbali bila kuathiri uhifadhi hasa wa mazingira na hifadhi za misitu tulizonazo.Ameongeza lengo la tatu lilikuwa kusikiliza kero na Changamoti za wananchi.

 "Kero karibu zote zilijibiwa palepale kwani wakuu wa idara zote na kamati ya ulinzi na usalama walikuwepo."Kwa kata ambazo nilikua nimekwenda kwa mara ya pili, lengo namba moja lilikua kuhamasisha uhifadhi na lengo namba mbili lilikua kujibu kero na changamoto za wananchi walizotoa katika mkutano uliopita ambazo hazikuwa zimetolewa majibu ya moja kwa moja.

" Lengo la tatu lilikua kusikiliza kero na changamoto nyingine za wananchi,"amefafanua.Ameeleza kuwa kuna kero ambazo zilitolewa majibu katika ziara iliyopita na kuna nyingine zilihitaji ufuatiliaji ikiwamo ya mgambo na wakulima wa korosho ambapo aliwapatia majibu.

Kuhusu mgambo Mkuu wa Wilaya Kizigo amesema wananchi wa Magazini katika kijiji cha Magazini walilalamika kwamba wao hawafanyiwi mafunzo ya mgambo hivyo kusababisha wakati wa kazi mbalimbali kama usimamizi wa mitihani wanakosa nafasi hizo. Majibu ndio hayo
 MKUU wa Wilaya ya Namtumbo Sophia Kizigo akiwasili kwenye moja ya kata wakati wa ziara yake alioyoifanya hivi karibuni wilayani humo,nana kutoa ufafanuzi kuhusu ziara hiyo ikiwemo kusikiliza changamoto za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.
 Baadhi ya Wananchi wakimsikiliza MKUU wa Wilaya ya Namtumbo, Sophia Kizigo (wa tatu kulia) alipokuwa akizungumza nao kwenye moja ya mkutano wake wa hadhara,katika kuzisikiliza changamoto za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...