Na Said Mwishehe, Globu ya jamii.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Ndege la Emirates nchini Tanzania Rashed Alfajeer amesisitiza kuendelea kutoa huduma bora kwa wateja wanaosafiri na ndege zao katika mataifa mbalimbali duniani.

Pia amezungumzia fursa zilizopo kutokana na uwepo wa safari za ndege zinazofanywa na Emirates kati ya Tanzania na nchi nyingine ikiwemo ya usafirishaji mizigo ya kibiashara kutoka Dar es Salaam ambako kumekuwa kituo kikubwa cha kibiashara kwa Afrika Mashariki.

Alfajeer amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati anazungumza na waandishi wa habari katika mazungumzo yaliyolenga kujenga uhusiano kati yake na vyombo vya habari kuhusu masuala ya kibashara na maisha.

“Emirates nia yetu ni kuendelea kuhakikisha wateja wetu wanakuwa wenye thamani bora kadri inavyowezekana,” amesema.

Hivyo wanaendelea kuwa wabunifu katika kutoa huduma bora zaidi. “Kila siku tumekuwa tukiangalia njia za ubunifu ili kuboresha huduma zetu kwa wateja ikiwa pamoja na kurahisi safari zao kati ya eneo moja ya jingine.”

Kuhusu mizigo amesema mingi kupitia Emirates kuna mizigo mingi ambayo inasafirishwa kutoka Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Ndege la Emirates nchini Tanzania Rashed Alfajeer akizungumza na Wanahabari jijini Dar es Salaam kuelezea mafanikio na jinsi wanavyoliendesha shirika hilo. Pembeni ni mmoja wa wafanyakazi wa shirika hilo, Tununu Kasambala. Picha na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
Mwandishi wa TBC1 Stanley Ganzel akiuliza swali. Waandishi wa habari wakifuatilia kwa makini mazungumzo ya Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Ndege la Emirates nchini Tanzania (hayupo pichani).
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Ndege la Emirates nchini Tanzania Rashed Alfajeer (wa sita kutoka kushoto) akiwa na wanahabari waliohudhuria mkutano wake. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...