Na Agness Francis,globu ya jamii
UONGOZI wa Singida United  wanategemea kukaa mezani na Mamelod  Sundowns  ya Afrika Kusini kwa ajili ya kufikia muafaka wa mchezaji Habibu Kyombo.

Mshambuliaji huyo kinara kwa ufungaji kwenye michuano ya Azam Sport Federation Cup aliekipiga  Singida United kwa msimu mzima uliopita 2017-18 amerejea nchini jana akitokea nchini humo.

Ambako alikuwa akifanya majaribio katika viwanja vya Schloorkop Mamelodi Sundowns kwa ajili ya majaribio kikosini hapo.

Imeelezwa Kyombo alipewa siku 10 za majaribio na uongozi wa klabu ya Mamelod na  kuongezewa tena siku zingine 10 kwa ajili ya kufanya trial na senior team.

Siku 20 zilipokamilika kwa majaribio ya mshambuliaji huyo huku mamelodi wakikikubali kiwango chake na uwezo wake mkubwa aliouonyesha kwa siku hizo alizopewa.

Baada ya kukaa mezani uwongozi wa Singada United na Mamelod Sundown kujadiliana kubaki  mchezaji huyo kwa waajiri wake  wa msimu uliopita au kujiunga na kikosi cha Mamelodi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...