Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. Abdul-Razaq Badru
Na Omega Ngole, Lilongwe,
TAASISI za kiserikali zinazotoa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu Afrika zinakutana kwa siku nne kuanzia kesho (Jumatatu, Septemba 24, 2018) mjini Lilongwe, Malawi katika mkutano ambao Bodi ya Mikopo ya Tanzania (HESLB) ikisema imejipanga kuchota mbinu za kuongeza ufanisi.

Mkutano huo wa kimataifa utafanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Bingu wa Mutharika na umeandaliwa na Shirikisho la Taasisi hizo linalofahamika kwa kifupi kama AAHEFA. Washiriki zaidi ya 160 kutoka nchi 11 na wadau mbalimbali kama Benki ya Dunia, USAID wanatarajiwa kushiriki.

Washiriki hao ni maafisa wa Serikali, Watendaji Wakuu wa taaasisi hizo zinazotoa mikopo na wageni waalikwa kutoka Tanzania, Kenya, Rwanda, Ghana, Uganda and Zambia. Wengine wanatoka Botswana, Lesotho, Namibia, Afrika Kusini na wenyeji Malawi.

Mkutano huo utafunguliwa kesho (Jumatatu, Sept 24, 2018) na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia wa Malawi Bw. Bright Msaka.

Akiongea mjini hapa kuhusu mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. Abdul-Razaq Badru ingawa HESLB imepata mafanikio makubwa karika kipindi cha miaka mitatu iliyopita, bado kuna nafasi kubwa ya kujifunza kutoka kwa nchi nyingine hususan za kiafrika ambazo zinakutana na changamoto kama za Tanzania.

“Katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita tumekusanya zaidi ya TZS 298 bn kati ya TZS 398 bn zilizokusanywa tangu kuanzishwa kwa HESLB mwaka 2005 … na kwa miongozo tunayopata kutoka Serikalini, tumefanikiwa kushughulikia malalamiko ya wanafunzi kwa kiasi kikubwa… ni lengo letu kutenda bora zaidi,” amesema Bw. Badru katika mkutano na wanahabari mjini Lilongwe leo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...