MPAKA TUTAKAPOKUTANA TENA KWENYE MAHALI PENYE ENZI NA UTUKUFU


 Mama Fortunata Joseph Msoka; tunakumbuka muda wote tulipokuwa nawe tukifurahi pamoja. Tunatamani Mungu angetupa upendeleo ukarudi hata kwa muda tu tukakaa na kuzungumza kama ulivyokuwa ukifanya; ukitufundisha mema, kushika Imani na kuwapenda ndugu na marafiki. 

Kwa hakika ulikuwa mtu pekee sana katika maisha yetu sisi watoto wako. 

Ni miaka mitano sasa lakini bado hatujaamini kweli umeondoka kwenye maisha yetu. Kila tukikuita hauitiki, tukija nyumbani haupo; ni ukweli ambao ni mchungu kumeza na maumivu yasiyoisha. Daima utadumu kwenye mioyo yetu watoto wako Paul na Constatine Msoka, Jackiline na Rose Mdami. 

Wajukuu wamekosa wa kumtania wamebaki kulibeba jina lako kwenye nyoyo zao. Hakika upendo wako hauta sahaulika kwa watu wote ulioshi nao; majirani, marafiki, WAWATA Parokia ya Ukonga na wanafunzi wako. 
Tunasema Buriani uendelee kulala usingizi wa Amani na Mungu Mwenyezi akaitulize roho yako na ya Baba yetu mahali pema Mbingun - Amina 

 Ufunuo 21:4 “ naye atafuta kila chozi katika macho yao wala mauti haitakuwapo tena, wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwepo tena, kwakuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita”

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...