Na Ripota Wetu,Globu ya jamii


MABONDIA 18 leo wanatarajia kupanda ulingoni katika ukumbi wa ulingo wa CCM Mwinjuma uliopo Mwananyamala kuwania mataji mbalimbali katika mchezo wa ngumi likiongozwa na pambano la raundi 10 kati ya Bushiri Kulwa na Seba.

Mapambano hyao yaliyoandaliwa na Kampuni ya ‘Golden Boy Africa’ yanawakutaniosha mabondia hao wanaowania mkanda wa Dunia katika uzito wa kilo 84 ‘Cruiser weights’ linatajwa kuwa la kipekee na hasa kutokanana na viwango walivyonavyo mabondia wote wawili katika medani ya ‘masumbwi’

Mbali na pambano hilo ,.michezo mingine inatarajiwa kuwakutanisha mabondia Simba na Allen, Chidi Mbishi dhidi ya Moro Best,Mkalekwa Junior dhidi ya Abdala Luwanje, Hamisi Maya dhidi ya Karage Suba itakayochezwa kwa raundi nane kila mmoja.

Mapambano mengine ambayo ni pamoja na bondia Mbunju Laga dhidi ya Iman Tavez, Nurdin Mohammed dhidi ya Issa Mbwana , Mlekwa dhidi ya Rama, pamoja na pambano kati ya Modest John dhidi ya Kassim Juma, yote yakichezwa kwa raundi 6.

Mratibu wa mapambano hayo Shomari Kimbau, alisema tayari maandalizi yote yamekwisha fanyika ikiwemo mabondia kupima afya zao kabla ya mchezo na kwamba kinachosubiriwa na kutimia kwa muda husika.

Alisema ‘mpambano’ huo unaotarajiwa kuanza saa 10 za jioni, unatarajiwa kuwa wa kuwa na ushindani mkubwa kutoka kwa mabondia wote, hasa kutokana na namna ambavyo kila kambi ya mabondia hao iolivyojipanga ili kupata ushindi.

Awataka wananchi kujitokeza kwa wingi ili kushuhudia vipaji kutoka kwa mabondia mbalimbali wa hapa nchinim huku akisisitiza uwepo wa suala la ulinzi na usalama kwa mashabiki watakaojitokeza kutazama pambano hilo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...