Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU) Profesa Evaristo Liwa akiongea machache wakati wa ufunguzi wa semina ya wiki mbili ya washiriki wa kozi ya kimataifa kuhusu maafa inayondeshwa na Chuo Kikuu Ardhi ikiwalenga wanafunzi wa shahada za juu na watendaji wa taasisi za kiserikali, binafsi na mashirika ya kimataifa jijini Dar es Salaam. Washiriki wanatoka nchi 12 za Afrika na Taasisi ya World Food Programme (WFP) Wakufunzi wanatoka Vyuo Vikuu vya Afrika vinavyounda mwamvuli wa Periperi U, UNDP na WHO Kozi hiyo imefadhiliwa na UNDP, USAID, WHO na WFP. Kushoto ni Kaimu Naibu Mkuu Chuo Mipango, Fedha na Utawala, Profesa Robert Kiunsi. (Picha na Robert Okanda)
Sehemu ya washiriki wa semina ya kozi ya mafunzo ya mbinu za namna ya kutathmini athari zitokanazo na maafa wakifuatilia matukio wakati wa ufunguzi wa semina hiyo Dar es Salaam leo Septemba 10 2018.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...