Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
SERIKALI imesema imejipanga vema kuhakikisha sekta ya nishati na hasa ya mafuta na gesi inawanufaisha Watanzania wote na kwamba nchi imefanya maandalizi makubwa kwa ajili ya kunufaika na sekta hiyo.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira na Muungano January Makamba wakati anafungua kongamano la pili la wadau wa sekta ya mafuta na gesi wakati anamwakilisha mgeni rasmi Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Kongamano hilo limehudhuriwa na zaidi ya wadau 200 kutoka mataifa zaidi ya 75 duniani na moja ya ajenda ni kuangalia fursa ambazo zinaweza kupatikana katika sekta ya mafuta na gesi huku pia kongamano hilo likijita kuangalia fursa ambazo watanzania watanufaika nazo kutokana na uwepo wa miradi mikubwa inayoendelea nchini.

Hivyo Waziri Januari Makamba amesema ujumbe wa Waziri Mkuu katika kongamano hilo ni kwamba nchi imefanya maandalizi makubwa kwa ajili ya kunufaika na sekta ya gesi na mafuta.

"Pia Serikali imeweka maandalizi ya kutosha ikiwa ni pamoja na kuandaa rasilimali watu, miundombinu, watalaamu na mambo mengine muhimu kwa lengo la kuhakikisha sekta hiyo inawanufaisha Watanzania wote,"amesema Januari Makamba.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira na Muungano January Makamba akizungumza wakati akifungua kongamano la pili la wadau wa sekta ya mafuta na gesi jijini Dar es Salaam leo kuhusu kongomano la wadau wa mafuta na gesi.
Waziri wa wizara ya Ardhi, nyumba, maji, nishati na mazingira Zanzibar, Salama Aboud Talib akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu kongomano la wadau wa mafuta na gesi.
Naibu waziri wa wizara ya nishati, Subira Mgalu akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu kongomano la wadau wa mafuta na gesi.
Muandaaji wa kongamano la mafuta na gesi ambaye pia ni Mwanzilishi na Makamu Mwenyekiti wa Shirikisho la Watoa Huduma za Mafuta na Gesi nchini Tanzania Abdulsamad Abdulrahim akifafanua jambo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...