Na Tiganya Vincent
Mkuu wa Utumishi Jesheni Meja Jenerali  Blasius Kalima Masanja amevipongeza vyombo vya ulinzi na usalama na viongozi wa Serikali Mkoani Tabora kwa kufanya kazi zao kwa ushirikiano ambao umesaidia kuimarisha ulinzi wa wananchi na mali zao.

Alisema vyombo hivyo vinapaswa kuwa kitu kimoja jambo ambalo litawasaidia kubadilishana taarifa ili kufichua vikundi vya kihalifu kwa ajili ya kuhakikisha amani na salama miongoni mwa wananchi.

Mkuu wa Utumishi Jesheni Meja Jenerali  Masanja alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na Viongozi wa Serikali , Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Mkoa na Maofisa wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania alipotembelea Ofisi ya Mkoa wa Tabora.

“Sio kila chombo kiende njia yake lazima kuwepo na umoja na mshikamano katika kuhakikisha ulinzi na usalama wa nchi” alisema.

Aliongeza kuwa na kila  Wananchi analo jukumu la kuhakikisha ulinzi na usalama wa nchi kwa kuchukua hatua za kutoa taarifa juu ya  vikundi vya uhalifu katika maeneo yao ambazo zitaviwezesha vyombo vya ulinzi na usalama kuchukua hatua za kuzuia uhalifu.
 Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Msalika Makungu akimkaribisha Mkuu wa Utumishi Jesheni Meja Jenerali  Blasius Kalima Masanja ili aweze kuzungumza na viongozi mbalimbali na Maofisa wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wakati alipotembelea Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Tabora. 
 Mkuu wa Utumishi Jesheni Meja Jenerali  Blasius Kalima Masanja akizungumza na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Tabora Kitwala Komaya(kushoto) , Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Msalika Makungu(kulia) na Maofisa wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wakati alipotembelea Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Tabora. 
Mkuu wa Wilaya ya Tabora Kitwala Komaya akuzungumza na viongozi mbalimbali na Maofisa wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wakati wa Mkuu wa Utumishi Jesheni Meja Jenerali  Blasius Kalima Masanja alipotembelea Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Tabora.
 Maofisa wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Tabora wakisikiliza Mkuu wa Utumishi Jesheni Meja Jenerali  Blasius Kalima Masanja (hayupo katika picha) wakati alipotembelea Ofisi ya  Mkuu wa Mkoa wa Tabora.
 Mkuu wa Utumishi Jesheni Meja Jenerali  Blasius Kalima Masanja akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Tabora Kitwala Komaya( wa tatu kutoka kushoto) , Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Msalika Makungu ( wa tatu kutoka kulia) na Maofisa wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa mara baada ya kutembelea Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Tabora.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...